-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa mwenye kutafuta riziki ya halali
Usiache kutafuta riziki kwa njia ya halali; kwani ni auni (msaada) kwa ajili yako katika dini.
-
Hadithi ya leo:
DiniUsichokipenda (kufanyiwa) wewe, usipende pia wafanyiwe wengine
Muadilifu zaidi miongoni mwa watu ni mwenye kuwapendelea watu yale anayoyapenda kwa ajili ya nafsi yake, na mwenye kuchukia (yasiwafike) watu yale anayochukia kwa ajili ya nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
DiniAmejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa
Amejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa, na atakuwa ameridhika na udhalili mwenye kufichua matatizo yake, na ambaye anauacha ulimi wake kuitawala roho yake ameishusha hadhi nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa hivyo katika fitina
Katika fitina kuwa kama mwana wa ngamia; Hana mgongo wa kupandwa wala chuku ili akamuliwe maziwa.
-
Hadithi ya leo:
DiniKwa kumfurahisha mwanao, mfurahishe pia Mwenyezi Mungu
Mwenye kumfundisha mtoto wake Qur'an, basi mtoto huyo ataitwa [Siku ya Kiyama] pamoja na wazazi wake na kuwavisha mavazi mawili ambapo nyuso za watu wa peponi zitang'aa kutokana na nuru yao.
-
Hadithi ya leo:
DiniWeka mambo yako katika mkondo wa haki
Hakuacha haki mwenye izza (heshima) isipokuwa alidhalilishwa, na dhalili hakuchukua haki isipokuwa alipata izza (heshima).
-
Hadithi ya leo:
DiniImamu Hussein (a.s): Acha maisha ya kidhalili
Kifo cha heshima ni bora kuliko maisha ya kidhalili. Mauti ni bora kuliko kuhusishwa na udhalili, na udhalili ni bora kuliko kuingia Motoni.
-
Hadithi ya leo:
DiniLipe uzito suala la heshima na ridhaa ya mwenza
Hakika aliye mbora zaidi miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule ambaye anamheshimu zaidi mwenza wake.
-
Hadithi ya leo:
DiniSema haki, kwani kuokoka kwako kuko katika hilo
Mche (muogope) Mwenyezi Mungu na sema haki hata kama utaangamia, kwani (kwa hakika) kuokoka kwako kuko katika hilo. Mche Mwenyezi Mungu na acha batili hata kama kuokoka kwako kuko katika hilo,…
-
Hadithi ya leo:
DiniKatu usifanye khiana katika amana
Mcheni Mwenyezi Mungu na rudisheni amana kwa yule aliyekuaminini.
-
Hadithi ya leo:
DiniJipambe kwa tabia njema
Tabia njema ni; Kumsamehe aliyekudhulumu, kuunga udugu aliyekukatia (udugu), kumpa aliyekunyima na kusema haki hata kama ni kwa madhara yako.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa hivi kwa watu
Kuwa mlaini kwa watu, kuwa na maneno mazuri na kutana na ndugu yako kwa bashasha na tabasamu.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa mtu wa utani (mzaha), lakini chunga mpaka wake
Mwenyezi Mungu anampenda afanyae mzaha katika mkusanyiko, kwa sharti asitukane na kutoa maneno machafu.
-
Hadithi ya leo:
DiniUsicheleweshe kulipa ujira wa kibarua
Mlipe kibarua kabla jasho lake halijakauka.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa hivi katika biashara
Yeyote anayefanya biashara (anauza na kununua) lazima aepuke vitu vitano, kinyume na hivyo asinunue au kuuza kabisa: Riba, kuapa, kuficha ubovu (wa bidhaa), kusifu bidhaa anazouza, na kukashifu…
-
Hadithi ya leo:
DiniChunga (mazingira) asili
Itakapowadia Siku ya Kiyama na mmoja wenu akawa ana mche mkononi mwake, akiweza kuupanda kabla ya kusimama Kiyama, basi aupande.
-
Hadithi ya leo:
DiniNi wajibu kwako kuchunga haki za kila mtu (awe Muislamu au sio Muislamu)
Kuna makundi mawili ya watu: Ama ni ndugu yako katika dini, au anayefanana na wewe katika uumbaji; kwa hali yoyote, unapaswa kuheshimu haki zao.
-
Hadithi ya leo:
DiniChunga vitendo vyako
Tambua kwamba, hautasalimika katu na jicho la Allah, basi tazama jinsi unavyotenda.
-
Hadithi ya leo:
DiniWeka kando tabia ya kujiona
Kujiona (kujikweza) kunamkwaza mtu kutafuta elimu na kunaleta udhalili na ujahil.
-
Hadithi ya leo:
DiniOgopa kilio na laana ya aliyedhulumiwa
Ogopa kilio na laana ya aliyedhulumiwa (madhulumu), hata akiwa kafiri, kwa sababu hakuna kizuizi dhidi ya laana ya aliyedhulumiwa.
-
Hadithi ya leo:
DiniChunga haki za wanyama
Kila unapowakabidhi wanyama kwa mtu mwaminifu, muagizie asitengananishe kati ya ngamia na mtoto wake, na asikamue maziwa yake kiasi cha kumdhuru mtoto... .
-
Hadithi ya leo:
DiniUsipuuze sauti ya wengine ya kuomba msaada
Mwenye kusikia sauti ya mwenye kuomba msaada na asiende kumsaidia, huyo sio Muislamu.
-
Hadithi ya leo:
DiniTanguliza utakasifu (kujiheshimu) katika kuamiliana na asiyekuwa maharimu
Kuweni na utakasifu (jiheshimuni) kwa wanawake wa watu, ili wanawake wenu wafanyiwe utakasifu (waheshimiwe).
-
Hadithi ya leo:
DiniTambua haki za watu na uzitekeleze
Daraja (cheo) ya juu mbele ya Mwenyezi Mungu ni ya mtu anayetambua haki za watu na akafanya juhudi zote kutimiza haki zao.
-
Hadithi ya leo:
DiniChunguza dafina (hazina) za Qur'ani
Aya za Qur'an ni dafina (hazina), na hazina inapofunguliwa, unapaswa kuona kilichomo ndani yake.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa katika orodha ya waja wema kabisa wa Mwenyezi Mungu
Ni wale ambao wanapofanya jema hufurahi, watendapo (jambo) baya huomba maghufira, wakipewa kitu hushukuru, na wakifikwa na majaribu (mtihani) huonyesha subira na wanapokasirika husamehe.
-
Hadithi ya leo:
DiniAmiliana na watu tofauti namna hii
Suhubiana na mtawala (mfalme) kwa hofu na tahadhari, na rafiki kwa unyenyekevu na bashasha, na adui kwa namna ambayo hoja yako kwake imetimia.
-
Hadithi ya leo:
DiniKuwa hivi wakati wa hasira, wa kuridhia na kuwa na nguvu
Muumini anapokasirika, hasira yake haimuondoi katika haki.
-
Hadithi ya leo:
DiniOndoa kinyongo kwa kutoa zawadi
Peaneni zawadi mpendane; kwani zawadi huondoa vinyongo (chuki).
-
Hadithi ya leo:
DiniUsiruhusu aone haya
Tafuta udhuru kwa neno na kitendo kibaya alichokifanya ndugu yako, na kama hukupata, mtafutie udhuru (ili asione haya).