تیتر سه زیرسرویس
-
Hadithi ya leo:
Kuwa mwenye kutafuta riziki ya halali
Usiache kutafuta riziki kwa njia ya halali; kwani ni auni (msaada) kwa ajili yako katika dini.
-
Hadithi ya leo:
Usichokipenda (kufanyiwa) wewe, usipende pia wafanyiwe wengine
Muadilifu zaidi miongoni mwa watu ni mwenye kuwapendelea watu yale anayoyapenda kwa ajili ya nafsi yake, na mwenye kuchukia (yasiwafike) watu yale anayochukia kwa ajili ya nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
Amejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa
Amejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa, na atakuwa ameridhika na udhalili mwenye kufichua matatizo yake, na ambaye anauacha ulimi wake kuitawala roho yake ameishusha hadhi nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivyo katika fitina
Katika fitina kuwa kama mwana wa ngamia; Hana mgongo wa kupandwa wala chuku ili akamuliwe maziwa.
-
Hadithi ya leo:
Kwa kumfurahisha mwanao, mfurahishe pia Mwenyezi Mungu
Mwenye kumfundisha mtoto wake Qur'an, basi mtoto huyo ataitwa [Siku ya Kiyama] pamoja na wazazi wake na kuwavisha mavazi mawili ambapo nyuso za watu wa peponi zitang'aa kutokana na nuru yao.
-
Hadithi ya leo:
Weka mambo yako katika mkondo wa haki
Hakuacha haki mwenye izza (heshima) isipokuwa alidhalilishwa, na dhalili hakuchukua haki isipokuwa alipata izza (heshima).
-
Hadithi ya leo:
Imamu Hussein (a.s): Acha maisha ya kidhalili
Kifo cha heshima ni bora kuliko maisha ya kidhalili. Mauti ni bora kuliko kuhusishwa na udhalili, na udhalili ni bora kuliko kuingia Motoni.
-
Hadithi ya leo:
Lipe uzito suala la heshima na ridhaa ya mwenza
Hakika aliye mbora zaidi miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule ambaye anamheshimu zaidi mwenza wake.
-
Hadithi ya leo:
Sema haki, kwani kuokoka kwako kuko katika hilo
Mche (muogope) Mwenyezi Mungu na sema haki hata kama utaangamia, kwani (kwa hakika) kuokoka kwako kuko katika hilo. Mche Mwenyezi Mungu na acha batili hata kama kuokoka kwako kuko katika hilo,…
-
Hadithi ya leo:
Katu usifanye khiana katika amana
Mcheni Mwenyezi Mungu na rudisheni amana kwa yule aliyekuaminini.
-
Hadithi ya leo:
Jipambe kwa tabia njema
Tabia njema ni; Kumsamehe aliyekudhulumu, kuunga udugu aliyekukatia (udugu), kumpa aliyekunyima na kusema haki hata kama ni kwa madhara yako.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivi kwa watu
Kuwa mlaini kwa watu, kuwa na maneno mazuri na kutana na ndugu yako kwa bashasha na tabasamu.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa mtu wa utani (mzaha), lakini chunga mpaka wake
Mwenyezi Mungu anampenda afanyae mzaha katika mkusanyiko, kwa sharti asitukane na kutoa maneno machafu.
-
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivi katika biashara
Yeyote anayefanya biashara (anauza na kununua) lazima aepuke vitu vitano, kinyume na hivyo asinunue au kuuza kabisa: Riba, kuapa, kuficha ubovu (wa bidhaa), kusifu bidhaa anazouza, na kukashifu…
-
Hadithi ya leo:
Chunga (mazingira) asili
Itakapowadia Siku ya Kiyama na mmoja wenu akawa ana mche mkononi mwake, akiweza kuupanda kabla ya kusimama Kiyama, basi aupande.
-
Hadithi ya leo:
Ni wajibu kwako kuchunga haki za kila mtu (awe Muislamu au sio Muislamu)
Kuna makundi mawili ya watu: Ama ni ndugu yako katika dini, au anayefanana na wewe katika uumbaji; kwa hali yoyote, unapaswa kuheshimu haki zao.
-
Hadithi ya leo:
Chunga vitendo vyako
Tambua kwamba, hautasalimika katu na jicho la Allah, basi tazama jinsi unavyotenda.
-
Hadithi ya leo:
Weka kando tabia ya kujiona
Kujiona (kujikweza) kunamkwaza mtu kutafuta elimu na kunaleta udhalili na ujahil.
-
Hadithi ya leo:
Ogopa kilio na laana ya aliyedhulumiwa
Ogopa kilio na laana ya aliyedhulumiwa (madhulumu), hata akiwa kafiri, kwa sababu hakuna kizuizi dhidi ya laana ya aliyedhulumiwa.