تیتر سه زیرسرویس
-
Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Imam Kadhim (a.s):
Imamu Kadhim (a.s): Kuwa jirani mzuri
Kuwa jirani mzuri hakuna maana ya kutomuudhi jirani, bali ujirani mwema (mzuri) ni subira yako kwa maudhi ya jirani.
-
Hadithi ya leo:
Daima kuwa mtu huru
Usiwe mtumwa wa mwingine, ilihali Mwenyezi Mungu amekuumba ukiwa huru.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa katika orodha ya waja wema kabisa wa Mwenyezi Mungu
Ni wale ambao wanapofanya jema hufurahi, watendapo (jambo) baya huomba maghufira, wakipewa kitu hushukuru, na wakifikwa na majaribu (mtihani) huonyesha subira na wanapokasirika husamehe.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivi katika maingiliano na watu
Ingilianeni na watu kwa namna ambayo mkifa wakulilieni, na mkiwa hai (na ikawa hawajakuoneni kwa muda) wawe na shauku ya kukuoneni.
-
Hadithi ya leo:
Ifundishe familia yako maamrisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu
Katika kauli yake Mwenyezi Mungu ulotukuka utajo wake "ziokoeni nafsi zenu na familia zenu na moto" wakauliza: Vipi tutaokoa (tutazikinga) familia zetu? akasema: Mnawaamrisha (yale ayapendayo…
-
Hadithi ya leo:
Acha matamanio ambayo yanakusababishia udhalili
Ni ubaya na uchafu ulioje kwa Muumini kufuata matamanio ambayo yanamsababishia udhalili.
-
Hadithi ya leo:
Jipambe kwa tabia njema
Tabia njema ni; Kumsamehe aliyekudhulumu, kuunga udugu aliyekukatia (udugu), kumpa aliyekunyima na kusema haki hata kama ni kwa madhara yako.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa mwenye kutafuta riziki ya halali
Usiache kutafuta riziki kwa njia ya halali; kwani ni auni (msaada) kwa ajili yako katika dini.
-
Hadithi ya leo:
Usichokipenda (kufanyiwa) wewe, usipende pia wafanyiwe wengine
Muadilifu zaidi miongoni mwa watu ni mwenye kuwapendelea watu yale anayoyapenda kwa ajili ya nafsi yake, na mwenye kuchukia (yasiwafike) watu yale anayochukia kwa ajili ya nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
Amejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa
Amejidharau mwenyewe yule mwenye kuwa na tamaa, na atakuwa ameridhika na udhalili mwenye kufichua matatizo yake, na ambaye anauacha ulimi wake kuitawala roho yake ameishusha hadhi nafsi yake.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivyo katika fitina
Katika fitina kuwa kama mwana wa ngamia; Hana mgongo wa kupandwa wala chuku ili akamuliwe maziwa.
-
Hadithi ya leo:
Kwa kumfurahisha mwanao, mfurahishe pia Mwenyezi Mungu
Mwenye kumfundisha mtoto wake Qur'an, basi mtoto huyo ataitwa [Siku ya Kiyama] pamoja na wazazi wake na kuwavisha mavazi mawili ambapo nyuso za watu wa peponi zitang'aa kutokana na nuru yao.
-
Hadithi ya leo:
Weka mambo yako katika mkondo wa haki
Hakuacha haki mwenye izza (heshima) isipokuwa alidhalilishwa, na dhalili hakuchukua haki isipokuwa alipata izza (heshima).
-
Hadithi ya leo:
Imamu Hussein (a.s): Acha maisha ya kidhalili
Kifo cha heshima ni bora kuliko maisha ya kidhalili. Mauti ni bora kuliko kuhusishwa na udhalili, na udhalili ni bora kuliko kuingia Motoni.
-
Hadithi ya leo:
Lipe uzito suala la heshima na ridhaa ya mwenza
Hakika aliye mbora zaidi miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule ambaye anamheshimu zaidi mwenza wake.
-
Hadithi ya leo:
Sema haki, kwani kuokoka kwako kuko katika hilo
Mche (muogope) Mwenyezi Mungu na sema haki hata kama utaangamia, kwani (kwa hakika) kuokoka kwako kuko katika hilo. Mche Mwenyezi Mungu na acha batili hata kama kuokoka kwako kuko katika hilo,…
-
Hadithi ya leo:
Katu usifanye khiana katika amana
Mcheni Mwenyezi Mungu na rudisheni amana kwa yule aliyekuaminini.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa hivi kwa watu
Kuwa mlaini kwa watu, kuwa na maneno mazuri na kutana na ndugu yako kwa bashasha na tabasamu.
-
Hadithi ya leo:
Kuwa mtu wa utani (mzaha), lakini chunga mpaka wake
Mwenyezi Mungu anampenda afanyae mzaha katika mkusanyiko, kwa sharti asitukane na kutoa maneno machafu.
-