Jumanne 18 Machi 2025 - 05:51
Uzinduzi wa tafsiri ya Qur'ani tukufu kwa Kiswahili iliyoandikwa na sheikh Hassan Ally Mwalupa

Tafsiri ya Qur'ani tukufu iliyoandikwa na sheikh Hassan Ally Mwalupa ni hazina ya kipekee inayowezesha waumini kuelewa na kutafakari ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa lugha nyepesi na fasaha.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Hawza, mradi huu umechapishwa na Al-Hitra Foundation, chini ya Mwenyekiti wake Alhaj Mehboob Somji, ikiwa ni juhudi kubwa za kueneza elimu ya Qur’an na kukuza uelewa wa dini kwa jamii.

Hafla hii adhimu imehudhuriwa na viongozi mashuhuri akiwemo Alhaj Mohamedraza M Dewji, Rais wa Khoja, pamoja na viongozi wa Bakwata, Maulamaa na Masheikh kutoka madhehebu yote ya Kiislamu. 

Hili ni tukio la kihistoria linalodhihirisha mshikamano wa Waislamu na umuhimu wa Qur’an katika maisha yetu. Kwa neema za Mwenyezi Mungu, Tafsiri hii itaongeza nuru ya elimu na kuimarisha imani zetu.

Uzinduzi wa kihistoria wa tafsiri ya Qur'ani kwa Kiswahili

Uzinduzi wa kihistoria wa tafsiri ya Qur'ani kwa Kiswahili

Uzinduzi wa kihistoria wa tafsiri ya Qur'ani kwa Kiswahili

Uzinduzi wa kihistoria wa tafsiri ya Qur'ani kwa Kiswahili

Uzinduzi wa kihistoria wa tafsiri ya Qur'ani kwa Kiswahili

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha