Jumatatu 31 Machi 2025 - 09:55
Visa za wanafunzi 300 wanaoipinga Israel katika vyuo vikuu vya Marekani zafutwa  

Marekani imefuta visa za wanafunzi wa kigeni 300 kwa sababu ya kushiriki maandamano ya kuunga mkono Palestina katika vyuo vikuu vya nchi hiyo.  

Kwa mujibu wa ripot kutoka katika watarjumu wa Shirika la Habari la HawzaMsako huu wa kuwakamata na kuwafukuza wanafunzi ni sehemu ya juhudi za serikali ya Donald Trump za kukandamiza wapinzani.  

Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, alieleza siku ya Alhamisi: “Tutafanya hivi kila siku, kila tunapompata mmoja wao tutaifuta visa yake, natumai siku moja watu hawa hawatakuwepo kabisa na tutakuwa tumewaondosha wote.

Kauli ya Rubio ilikuja baada ya kukamatwa kwa Romiz Ozturk, mwanafunzi wa udaktari kutoka Uturuki katika chuo kikuu cha Tufts, ambaye alikamatwa na maafisa wa uhamiaji karibu na nyumbani kwake Hapo awali, Ozturk alikuwa ameandika makala katika gazeti la chuo kikuu akiitaka taasisi hiyo kutambua vitendo vya utawala wa Israel huko Gaza kama mauaji ya kimbari.  

Miongoni mwa waliokamatwa mwezi uliopita ni Mahmoud Khalil, raia wa Palestina mwenye hadhi ya ukaazi wa kudumu, na Badrakhan Suri, mtafiti wa baada ya udaktari kutoka India.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha