Jumatatu 31 Machi 2025 - 09:58
Wosia wa kiroho wa Ayatollah Kishmiri kabla ya kulala

Hawza; Ayatollah Kishmiri usingizi anauona ni kama vile ndugu wa mauti, na anahusia mtu achukue udhu kabla ya kulala, alale akiwa ameelekea Qibla, na asome Ayat  Kursii, Tasbihi za bibi Zahra (a.s), na kufanya istighfār ili kupata usiku wenye utulivu.  

Kwa mujibu wa ripoti kutoka katika Shirika la Habari la Hawza, Wosia wenye thamani kutoka kwa Ayatollah Kishmiri kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kiroho kila usiku ulijikita zaidi kwenye kutumia njia hii.

Ayatollah Kashmiri alisema:
Ni muhimu kutambua kuwa usingizi ni mfano wa mauti, na kila unapofika usiku mtu inatakiwa ajitayarishe kwa jambo hili.

Kwa kuifanya upya imani na ahadi yake kwa Mungu, mtu anatakiwa kutawadha, kuelekea Qibla, na kulala akimtaja Mwenyezi Mungu, aanze kwa kusoma Ayat Kursii, kisha afuate kwa kusoma Tasbihi za Bibi Zahra (a.s), na mwishowe atake msamaha kwa Mwenyezi Mungu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha