Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, matini ya ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa taifa la Iran ni kama ifuatavyo:
Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu
Enyi taifa la Iran lenye hamasa na uaminifu!
Kama mlivyofahamishwa, mkataba wa maelewano umetiwa saini kati ya Rais wa Iran na Rais wa Marekani, katika njia ya kufikia hatua hii, viongozi husika walifanya juhudi nyingi kwa nia ya dhati na kwa mtazamo mwema, bila shaka alikuwa Rais wa Marekani ambaye, kutokana na hali ya kukata tamaa na kushindwa kwake, alikuwa akitumia aina mbalimbali za mbinu na nyenzo ili kufanikisha jambo hili.
Kwa msingi wa kanuni na mtazamo wangu wa awali, nilikuwa na maoni tofauti. Hata hivyo, kutokana na ahadi ambayo Mheshimiwa Rais, akiwa Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, kwa niaba yake mwenyewe na wanachama wengine, alinipa kuhusu kulinda haki za taifa la Iran na Kambi ya Muqawama, na akasisitiza kwamba anakubali kubeba jukumu la jambo hilo, nilitoa ruhusa ya kufanyika kwake.
Pia amesisitiza kwamba; ikiwa upande wa Marekani utataka kufanya madai ya kupita kiasi au kuonesha tamaa ya kuzidisha masharti, hawatakubali wala hawatajisalimisha mbele ya jambo hilo.
Kuanzia wakati huu, sisi yaani ninyi taifa lenye heshima na mimi mtumishi huyu mdogo, tutakuwa tukisubiri kutekelezwa kwa masharti yaliyotajwa, hata hivyo, ni jambo lililo wazi kwamba mazungumzo ya ana kwa ana yatakayofanyika hapo baadaye hayatamaanisha kukubali maoni au matakwa ya adui.
Tunatumaini kwamba dua njema za Bwana wetu, Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake kwa utukufu, zitaleta aina mbalimbali za nusura, ushindi na mafanikio kwa taifa la Iran lenye heshima.
Na amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka Zake.
Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei
28 Khordad 1405 H.Sh. (18 Juni 2026)
Maoni yako