Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, baada ya ushindi dhidi ya RC Strasbourg, wachezaji wa timu ya Rayo Vallecano kwa mara nyingine walionesha uhusiano wa kina kati ya michezo na ubinadamu katika kuunga mkono muqawama wa Palestina, kwa kuinua bendera ya Palestina katikati ya uwanja wa mchezo na kupaza sauti za kauli mbiu dhidi ya Uzayuni.
Timu hii sasa, ikiwa mwakilishi wa Hispania katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Europa, ilifanikiwa kumshinda mgeni wake Strasbourg kwa matokeo ya 1-0; hata hivyo, jambo lililoufanya ushindi huu kuwa gumzo katika vyombo vya habari vya dunia ni kitendo cha alama kilichofanywa na wachezaji mwishoni mwa mchezo.
Mara tu baada ya filimbi ya mwisho, mmoja wa wachezaji wa Rayo Vallecano alielekea upande wa mashabiki, akachukua bendera kubwa ya Palestina na akaipeperusha hadi mbele ya lango. Kitendo hiki, ambacho kiliambatana na shangwe endelevu za watazamaji, kilitoa ujumbe wazi wa mshikamano wa klabu hiyo na watu wa Ghaza, pamoja na kulaani uhalifu unaofanywa na utawala wa Kizayuni duniani kote.
Mwishoni mwa mchezo, mashabiki wa timu hiyo walionesha hasira zao dhidi ya uvamizi na mauaji ya kimbari nchini Palestina kwa kupaza sauti za kauli mbiu dhidi ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni.
Chanzo: Awa Press
Maoni yako