Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Hujjat al-Islam wal-Muslimin Mahdi Isma’ili, mkuu wa Hawza ya Kashan, katika mahojiano na mwandishi wa habari wa Shirika la Habari la Hawza mjini Kashan, alisema: Arubaini ya Husseini ni kilele cha mtiririko wa ushindi wa damu dhidi ya upanga, ushindi wa waliodhulumiwa dhidi ya madhalimu, na kushinda kwa fikra ya Husseini juu ya fikra ya Yazidi.
Fikra ya urekebishaji na kupinga ubeberu ya Imam Hussein (as)
Aliongeza: Fikra ya urekebishaji na kupinga ubeberu ya Hussein (as), kama vile ilivyoshinda katika Karbala dhidi ya fikra ya majeshi ya adui yaliyojaa silaha, hakika hadi kufikia ujio wa Mkombozi itazidi kuwa ya kimataifa na yenye kuunda harakati kila siku. Mto wa machozi ya wapendwa wa Hussein (as) na waliodhulumiwa duniani utazizamisha tawala za kidhalimu, kwa kuwa imeelezwa kuwa Hussein ni aliyeuawa kwa machozi.
Arubaini – Uwanja wa Ushindi wa Waliodhulumiwa
Mkuu wa hawza ya Kashan alisema kuwa ushiriki wa mamilioni ya Waislamu wa kishia katika Arubaini ya Husseini ni dhihirisho la uwanja wa kudhihiri na uwepo wa wapendwa na wafuasi wa fikra ya Husseini, na akakumbusha kuwa: Arubaini ni uwanja wa wafuasi ambao katika historia wametengwa na kudhulumiwa.
Alibainisha pia: Mtiririko wa Arubaini kwa hakika ni damu ya kiongozi wa mashahidi Imam Hussein (as) ambayo ujumbe wake kila mwaka kwa uwepo mpana wa tabaka mbalimbali za watu kutoka jukwaa hili la mamilioni, unapelekwa duniani na kupiga kelele kauli mbiu ya kupinga dhulma na ushindi wa damu juu ya upanga.
Maana ya Karbala zaidi ya Tukio la Kihistoria
Hujjat al-Islam wal-Muslimin Isma’ili alisema: Huenda kama wakati wa kutokea kwa tukio la Karbala mtu angeidai kuwa damu itashinda upanga na kuwa aliyedhulumiwa anaweza kushinda juu ya dhalimu, lingekuwa gumu kwa jamii ya Waislamu na wanyonge kuamini, kwa kuwa wanadamu wanahukumu kwa sura ya nje na kuchunguza tukio la Karbala kama tukio, si mtiririko wa fikra ya Aba - abdillah.*
Alisisitiza pia: Iwapo kwa mtazamo wa nje, Karbala itaangaliwa kama tukio, matokeo yake ni kuondolewa kwa kimwili kwa Aba-abdillah Hussein (as) na wafuasi wake. Lakini iwapo itaangaliwa kama kuanzishwa kwa mtiririko wa urekebishaji, upingaji wa dhulma na mapambano dhidi ya upotofu na ufisadi katika historia, hakika mtiririko wa Aba-abdillah katika historia umeshinda, umeendelea na ni wenye athari.
Ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Waliodhulumiwa
Mkuu wa hawza ya Kashan alisisitiza kwa kusema: Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Qur’ani Tukufu, kwa kuashiria azma ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya uongozi na utawala wa waliodhulumiwa duniani, anasema:
وَنُرِيدُ أَنْ نَمُنَّ عَلَى الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا فِي الْأَرْضِ وَنَجْعَلَهُمْ أَئِمَّةً
Na tukataka kuwafadhili walio dhoofishwa katika nchi hiyo na kuwafanya wawe waongozi na kuwafanya ni warithi.
(Qasas: 5)
Yaani azma ya hakika ya Mwenyezi Mungu ni kuwaneemesha waliodhulumiwa duniani na kuwafanya viongozi na warithi wa ardhi, hakika moja ya nyenzo muhimu za kuandaa uongozi huu ni mtiririko wa Aba-abdillah, Arubaini na kuandaa mtiririko wa uongozi wa waliodhulumiwa wa historia chini ya uongozi wa fikra ya Imam Hussein (as) na uongozi wa Mrekebishaji Mkuu, yaani Bwana wa Zama Mahdi (aj).
Mwisho wa ujumbe
Maoni yako