Alhamisi 16 Julai 2026 - 00:07
Kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi hakuhusiani na kubadilishana serikali au watu wanaohusika/ Makubaliano yamekwisha; mazungumzo yasiendelezwe/ Taifa la Iran halitatoa hongo kwa adui

Kwa mujibu wa ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, madai ya kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi pamoja na mashahidi wengine wa vita viwili vya karibuni ni jambo la lazima na la hakika, na hayahusiani na kubadilika kwa serikali au watu wanaohusika. Kwa hali yoyote ile, jambo hilo litatimizwa, na wahalifu pamoja na waliotekeleza jinai hizi, kuanzia sasa hawatawahi tena kujihisi salama. Bila shaka, matumaini yao ya kufa kwa utulivu wakiwa vitandani mwao yatazikwa pamoja nao kaburini. Kisasi hiki kitafuatiliwa katika uwanja wa kimataifa na kwa upana, kwa juhudi za wapenda uhuru duniani kote.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Alireza A'rafi, Mkurugenzi wa Hawza nchini Iran, ametoa tamko la uchambuzi lililofafanua ujumbe muhimu wa hafla za kuaga, kusindikiza na mazishi ya kihistoria ya Imam Shahidi yaliyohudhuriwa na mamilioni ya watu nchini Iran na Iraq.

Katika tamko hili la uchambuzi, Mkurugenzi wa Hawza nchini Iran, amegusia suala la kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi huku akisisitiza kwamba; kwa mujibu wa ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, madai ya kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi pamoja na mashahidi wengine wa vita viwili vya karibuni ni jambo la lazima na la hakika, na halihusiani na kubadilika kwa serikali au watu wanaohusika. Kwa hali yoyote ile, jambo hilo litatimizwa, na wahalifu pamoja na waliotekeleza jinai hizi, kuanzia sasa hawatawahi tena kujihisi salama. Bila shaka, matumaini yao ya kufa kwa utulivu wakiwa vitandani mwao yatazikwa pamoja nao kaburini. Kisasi hiki kitafuatiliwa katika uwanja wa kimataifa na kwa upana, kwa juhudi za wapenda uhuru duniani kote.

Makubaliano yamekwisha/ Mazungumzo yasiendelezwe

Mjumbe wa Baraza la Mafaqihi la Baraza la Kulinda Katiba pia ameashiria ukiukwaji wa mara kwa mara wa makubaliano kati ya Iran na Marekani uliofanywa na adui mhalifu. Kuhusiana na hilo amesema: "Sasa kwa kuwa adui, kupitia vitisho, matusi, mashambulizi ya kijeshi, kuendelea kwa vikwazo vya kiuchumi, kutolipa fidia, kutorejesha utajiri wa taifa, kutotekeleza usitishaji vita, pamoja na kutorudi nyuma Israel vamizi kutoka ardhi ya Lebanon, na baadaye kwa kurejesha mzingiro wa baharini dhidi ya Iran, amevunja vipengele vyote vya makubaliano hayo; na sasa kwa kuwa Rais wa Marekani ametangaza waziwazi na kwa jeuri kabisa kumalizika kwa makubaliano hayo na kuanzisha vita, basi hakuna tena msingi wa kushikamana na makubaliano hayo wala kuendelea na mazungumzo."

Ushauri wa Kimkakati kwa Viongozi Wakuu

Mheshimiwa Rais mwenyewe, ambaye kwa niaba ya wajumbe wa Shaam amejifunga mbele ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na mbele ya taifa shupavu na lenye msimamo la Iran kutekeleza vipengele vya makubaliano hayo na kusimama dhidi ya tamaa za Marekani, pamoja na wajumbe wengine wa Shaam, makamanda na viongozi wa diplomasia ya nchi, wanapaswa kuyahesabu makubaliano hayo kuwa yamekwisha, wachukue njia ya jihadi na kusimama imara, na kwa utiifu kamili kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu warejee katika njia ile ambayo yeye ameiona kuwa sahihi.

Ayatullah A'rafi amesisitiza kwa nguvu jambo hili muhimu kwamba taifa kubwa la Iran haliko tayari kutoa hongo kwa adui kwa sababu ya matatizo ya kiuchumi, bali liko tayari kujitolea hadi tone la mwisho la damu yake katika njia ya kuandaa mazingira ya kudhihiri kwa Imam Mahdi (as) na kufikia kilele cha ushindi.

Kwa hiyo, viongozi hawapaswi, kwa kisingizio cha matatizo ya kiuchumi, hofu ya gharama za vita, kushambuliwa kwa miundombinu na sababu nyinginezo, kuachana na haki halali za Umma wa Kiislamu, wala kuendelea zaidi na njia ya mazungumzo na makubaliano na makafiri ambao, kwa mujibu wa kauli ya Qur'ani Tukufu,

hawashikamani na ahadi yoyote: «لَا أَیْمَانَ لَهُمْ».

Lifuatalo ni tamko kamili la uchambuzi wa Mkurugenzi wa Hawza nchini Iran:

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

«مِنَ الْمُؤْمِنِینَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّهَ عَلَیْهِ فَمِنْهُمْ مَنْ قَضَیٰ نَحْبَهُ وَمِنْهُمْ مَنْ یَنْتَظِرُ وَمَا بَدَّلُوا تَبْدِیلًا»

Mazishi ya kihistoria na yasiyo na mfano ya Kiongozi Mkuu na Mtukufu wa Ulimwengu wa Uislamu, Ayatullah al-Udhma Imam Khamenei (ra), pamoja na baadhi ya wanafamilia wake, yaliyofanyika katika miji ya Tehran, Qom, Najaf Ashraf, Karbala Tukufu na Mashhad Tukufu, sambamba na mazishi ya mfano na kufanyika kwa majlisi za maombolezo katika nchi na maeneo mengi duniani, yameweka alama muhimu sana katika mwelekeo wa safari ya kuelekea ustaarabu mpya wa Kiislamu na kuandaa mazingira ya kudhihiri kwa Jua Kuu la Wilaya, Imam Mahdi Aliyeahidiwa (as).

Ushiriki wa makumi ya mamilioni ya watu waliobeba bendera nyekundu za kudai kisasi na kupaza sauti za kulipiza kisasi umegeuza mazishi hayo kuwa mazishi makubwa zaidi na yasiyo na mfano katika historia.

Mazishi haya yalikuwa ni dhihirisho la mapenzi yasiyo na mipaka ya watu kwa Walii wao; mapenzi ambayo Mwenyezi Mungu huwaweka waumini wenye imani na matendo mema ndani ya nyoyo za Waumini:

«إِنَّ الَّذِینَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَیَجْعَلُ لَهُمُ الرَّحْمَنُ وُدًّا»

Utawala wa hali ya mazishi hayo ulikuwa ni mchanganyiko wa huzuni nzito na hamasa kubwa ya kishujaa. Katika kumuaga Imam Shahidi wao, wananchi walionesha hisia na utambuzi wa Kihussein na Ashura. Hisia hizi zilizofurika zilikuwa ni dhihirisho la tabaka la ndani kabisa la utambulisho wao wa kiimani na kimapinduzi, na ni mtaji mkubwa kwa Mfumo wa Kiislamu ambao unapaswa kutumiwa katika kuendeleza harakati za kimapinduzi na kufanikisha malengo yake ya juu.

Mazishi haya makubwa, ambayo yaligeuka kuwa onyesho la nguvu la Umma wa Kiislamu na Mhimili wa Muqawama mbele ya kambi ya ukafiri na ubeberu, yalimkasirisha Rais wa Marekani mwenye matatizo ya kiakili na asiye na adabu, kutokana na hali ya kukata tamaa, alianza kutoa maneno ya kipuuzi, vitisho na matusi dhidi ya taifa kubwa la Iran. Katikati ya mazishi haya makubwa kwa mara nyingine tena alivunja ahadi aliyokuwa ameitoa katika makubaliano na kushambulia maeneo ya kusini na kaskazini mwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Aidha, katika siku za hivi karibuni ametangaza rasmi na wazi vita, na kuyashambulia kinyama maeneo mengi ya nchi. Hata hivyo, kwa upande mwingine alipokea mapigo makali na ya kuangamiza kutoka kwa vikosi vya kijeshi vyenye nguvu vya Iran.

Mazishi haya kwa mara nyingine yameudhihirishia ulimwengu mantiki ya ushindi wa damu dhidi ya upanga na roho ya kukikaribisha kifo na shahada iliyo ndani ya taifa la Iran na Mhimili wa Muqawama. Vilevile yameimarisha mantiki ya kauli mbiu ya "Tunaweza", yakaonesha nafasi isiyoweza kufidiwa ya irada, uwepo na mwamko wa wananchi katika kusimama imara, kustawi na kuendeleza nchi, na kuudhihirishia ulimwengu kwamba mwelekeo mpya wa mahusiano ya kimataifa uko katika mchakato wa kubadilika.

Bila shaka, onyesho hili la nguvu, mwamko na hamasa ya ajabu ya Umma wa Kiislamu katika mazishi ya Imam Shahidi, katika mazingira haya magumu sana ya vita mseto, limebeba ujumbe wa kina na wa kimkakati kwa viongozi, wananchi, Hawza, wanazuoni wenye kujitolea, Mhimili wa Muqawama na ulimwengu wa Kiislamu.

Sasa kwa kuwa Imam Shahidi, pamoja na miili hii mitakatifu na safi, wamepumzishwa kandokando ya Imam Mpole, Ali bin Musa Al-Ridha (as), basi mzigo mzito wa kuendeleza njia hadi kufikia kilele cha kudhihiri kwa Imam Mahdi (as) uko mabegani mwetu sote. Kufafanua ujumbe huu wa kimkakati kwa ajili ya kuendelea na safari hiyo hadi kufikia kilele hicho ni jambo la lazima.

Mimi, pamoja na kupongeza hamasa ya mamilioni ya wananchi na kutoa pole kwa Imam wa Zama (aj), na kwa Kiongozi wa Waislamu, Ayatullah Imam Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei (damat barakatuh), napenda kubainisha ujumbe wa kimkakati wa harakati hii kubwa ya kihistoria na kuwakumbusha wajibu ambao tunapaswa kuutekeleza kuanzia sasa na kuendelea.

Ujumbe wa Kudai Damu na Kulipiza Kisasi kwa Wauaji wa Imam Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu

Mazishi ya Imam Shahidi pamoja na bendera nyekundu za Ashura zilizokuwa zikipeperushwa mikononi mwa wananchi yalionesha wazi kwamba kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi ni haki ya kisheria na ya kisharia ya taifa hili pamoja na wapenda uhuru wote duniani. Katikati ya umati mkubwa wa walioshiriki mazishi hayo, kauli za "Kisasi!", "Ya Litharat al-Khamenei", pamoja na madai ya kuuawa kwa Trump na Netanyahu, zilisikika kwa nguvu zaidi kuliko wito mwingine wowote.

Kupepea kwa bendera nyekundu, ambazo katika utamaduni wa dini ni alama ya kudai damu na kulipiza kisasi, kulibeba ujumbe wa wazi na thabiti kwa maadui na wavamizi kwamba; taifa hili lina dhamira ya dhati ya kulipiza kisasi kwa damu safi ya Imam Shahidi wao na mashahidi wote wa vita hivi viwili kutoka kwa wauaji wahalifu na waliopoteza heshima.

Kulipiza Kisasi na Kudai Damu ya Imam Shahidi Hakuhusiani na Kubadilika kwa Serikali au Watu

Kama alivyosema Kiongozi wetu mpendwa katika ujumbe wake wa hivi karibuni kuhusu mazishi na maziko ya Shahidi wa Iran, kudai damu ya Imam Shahidi ambae aliishi kwa njia ya Imam Hussein (as) na akapata shahada kwa njia ya Imam Hussein (as), pamoja na kudai damu ya mashahidi waliouawa katika vita viwili vya karibuni vya kulazimishwa wakipigania njia ya Imam Hussein (as), ni mwendelezo wa kudai damu ya Imam Hussein (as) na masahaba wake, jambo ambalo limeelezwa wazi katika Dua ya Nudba na Ziara ya Ashura.

Kwa msingi huo kwa mujibu wa ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, madai ya kulipiza kisasi na kudai damu ya Imam Shahidi pamoja na mashahidi wengine wa vita viwili vya karibuni ni jambo la lazima na la hakika, na halihusiani na kubadilika kwa serikali au watu wanaohusika. Kwa hali yoyote ile, jambo hilo litatimizwa, na wahalifu pamoja na waliotekeleza jinai hizi, kuanzia sasa hawatawahi tena kujihisi salama. Bila shaka, matumaini yao ya kufa kwa utulivu wakiwa vitandani mwao yatazikwa pamoja nao kaburini. Kisasi hiki kitafuatiliwa katika uwanja wa kimataifa na kwa upana, kwa juhudi za wapenda uhuru duniani kote.

Vyombo vya habari vya kimataifa vimeelewa vyema kilio hiki kikubwa cha Umma wa Kiislamu na kukitafsiri kuwa ni "mazoezi ya kuonesha azma ya taifa", jambo ambalo litabadilisha mahesabu ya maadui. Adui huyu mhalifu na Yazidi wa zama hizi pia ametetemeshwa na ujumbe huu, kiasi kwamba ameongeza ulinzi wa viongozi na makamanda wake.

Bila shaka, adui atalazimika kulipa gharama ya jinai hii ili asije akathubutu tena kufanya kitendo kama hicho. Kuanzia sasa, wananchi wanapaswa kuendelea kuwasha moto huu wa kisasi ndani ya nyoyo zao hadi pale utakapotekelezwa kikamilifu, na kuugeuza kuwa azma ya kudumu ya kuifuata njia ileile ambayo Imam Shahidi aliinyunyizia kwa damu yake.

Muungano huu ni mtaji mkubwa kwa ulimwengu wa Kiislamu na ni jibu thabiti dhidi ya njama za maadui zinazolenga kuleta mgawanyiko. Ni wajibu kuulinda umoja huu na kuufanya uzidi kupanuka na kuimarika siku baada ya siku. Viongozi katika nyanja za kijeshi na diplomasia wanapaswa kuonesha uungaji mkono unaohitajika kwa Mhimili wa Muqawama, hususan nchini Iraq, Lebanon na Yemen. Wananchi nao wanapaswa kuendelea kudai na kuimarisha umoja huu zaidi kupitia uwepo wao mitaani.

Ujumbe wa Uhusiano Usiovunjika wa Wanazuoni na Uongozi pamoja na Wananchi

Uwepo wa kishindo na uliojitokeza wazi wa wanazuoni wa dini katika mazishi haya ya kihistoria, wakiwa katika nafasi ya utumishi, waongozaji na wasindikizaji wa wananchi, ulionesha uhusiano usiovunjika wa wanazuoni hao na Imam, Umma wa Kiislamu pamoja na Mhimili wa Muqawama. Hususan, ushiriki wa Maraji Wakuu wa Taqlid, wanazuoni mashuhuri na walimu wa Hawza za Qom na Najaf Ashraf katika hafla za mazishi ulidhihirisha uhusiano wa kina na usiovunjika wa Marjaiyya na wanazuoni wakubwa na uongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, wananchi na harakati za Muqawama.

Kwa miaka mingi adui ametambua umuhimu wa nafasi ya Maraji na wanazuoni katika kuendeleza malengo matukufu ya Mapinduzi ya Kiislamu. Tangu mwanzo wa Mapinduzi, amekuwa akijaribu kudhoofisha nafasi ya Marjaiyya na wanazuoni mbele ya wananchi kupitia mauaji ya kimwili, mauaji ya heshima na sifa, kupenyeza mawakala, pamoja na kueneza mifarakano na fitina ili kuzusha migawanyiko kati ya wanazuoni, Maraji na uongozi.

Ushiriki huu mkubwa wa wanazuoni, wasomi mashuhuri na Maraji Wakuu katika Swala ya Maiti na mazishi umeonesha kwamba mipango ya adui haijafanikiwa, na kwamba wanazuoni leo wako karibu zaidi na wananchi, wanawahudumia kwa moyo wote na wanaunga mkono uongozi kwa dhati.

Ni muhimu kwa Waumini na wanazuoni kuilinda dhamana hii takatifu, na wanazuoni waendelee kuimarisha na kupanua uhusiano huu siku baada ya siku kupitia huduma ya dhati na juhudi za kujitolea kwa wananchi.

Ujumbe wa Kufanya Upya Baia kwa Kiongozi Mwenye Hikima wa Mapinduzi na Kuuunga Mkono Mfumo wa Kiislamu

Katikati ya hamasa hii kubwa, kulifanyika "upigaji kura" wa kimya lakini wenye nguvu kubwa. Waislamu na wanamapinduzi wa Iran na ulimwenguni kote walifanya upya baia yao kwa Kiongozi mpya, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei. Baia hii ya makumi ya mamilioni ya watu, ambayo ilidhihirika katika njia yote ya mazishi kupitia kauli mbiu za "Roho yangu iwe fidia kwa Kiongozi" na "Labbayka Ya Khamenei", ilionesha kwamba uongozi mpya tangu mwanzo kabisa unaungwa mkono na umati mkubwa wa wananchi, na kwamba wananchi wanaendelea kuwa waaminifu kwa Mfumo wa Kiislamu unaojengwa juu ya Wilayatul Faqih.

Ahadi ya utii wa Umma kwa mrithi mwema wa Imam Shahidi kama Kiongozi wa Mfumo wa Kiislamu inatokana na utambuzi wa kipekee wa fikra ya Wilaya na Uimamu katika utamaduni wa kale wa Kishia, jambo ambalo litakuwa mwongozo katika safari ya kuelekea vilele vya utukufu na heshima ya Umma.

Baia hii, ambayo inahitaji utiifu kamili na uungaji mkono wa dhati kwa uongozi, itamuwezesha Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kuliongoza kwa nguvu zaidi jahazi la Mapinduzi hadi kulifikisha kwenye ufukwe mzuri wa kudhihiri Imam Mahdi (as).

Bila shaka, adui katika vita hivi vya mseto na vita vya kiakili atafanya kila juhudi kuivunja au kuidhoofisha ahadi hii. Wanazuoni wakuu na wananchi wenye kushikamana na Wilaya wanapaswa kueneza uelewa na kuongeza basira kupitia jihadi ya kubainisha ukweli ili kuvuruga mipango ya adui.

Ujumbe wa Kushikamana Umma na Uislamu pamoja na Maadili ya Kiislamu

Ushiriki mkubwa, wa hamasa na kishujaa wa wananchi, uliosheheni huzuni, majonzi na machozi katika mazishi ya Imam Shahidi ambaye alikuwa wa Kihussein, alifikiri kwa mtazamo wa Kihussein, alitembea katika njia ya Kihussein, alipigana jihadi na kusimama imara kwa njia ya Kihussein, aliishi maisha ya Kihussein, na akaitoa damu yake katika njia ya shule ya Imam Hussein (as), huku akitumia maisha yake yote kulinda misingi, kanuni, malengo, hukumu na maamrisho ya Uislamu pamoja na maadili ya Kimapinduzi, vilipeleka ujumbe kwa ulimwengu kwamba wananchi wamejizatiti kushikamana na Uislamu, maadili na hukumu zake, na wako tayari, kama Imam wao, kutoa maisha yao na ya watoto wao kwa ajili ya kuulinda Uislamu.

Kwa miaka mingi adui amefanya juhudi kubwa kupitia uvamizi wa kitamaduni, kueneza ufisadi wa maadili, uzembe wa kidini na kupenda dunia, kwa lengo la kubadili utamaduni wa jamii, kueneza mtindo wa maisha wa Kimagharibi na kuwatenganisha wananchi na Uislamu. Kwa kiwango fulani pia alifanikiwa, na mara nyingi Imam Shahidi alitahadharisha kuhusu hatari hii na kueleza wasiwasi wake.

Hata hivyo, ushiriki huu wa wananchi umeonesha kwamba kwa baraka za damu ya mashahidi wa vita hivi viwili, na hasa damu ya Imam Shahidi aliyedhulumiwa, wananchi sasa wameelekea kwenye Uislamu zaidi kuliko hapo awali kwa moyo wao wote, na kwamba damu hizi kwa kiwango kikubwa zimefanikiwa kuzima uvamizi wa kitamaduni wa adui.

Pamoja na hayo, hatari hii bado ipo, ni lazima viongozi wa masuala ya utamaduni nchini, wanazuoni wakuu na nguvu zote za Waumini na wanamapinduzi wajione kuwa na wajibu mbele ya tishio hili kubwa. Wanapaswa kutumia vizuri fursa iliyotolewa na damu hizi takatifu kupitia sera sahihi na zenye ufanisi za kiuchumi na kitamaduni, pamoja na jihadi ya kubainisha ukweli na uwasilishaji wazi na wenye mvuto wa ujumbe wa dini, ili kuvuruga mipango ya adui katika uwanja huu na kuharakisha safari ya kuelekea kuundwa kwa Umma wa Kiislamu na ustaarabu wa Kiislamu.

Ujumbe wa Fedheha na Kushindwa kwa Mipango na Njama za Adui

Sisi pia, kama Kiongozi wetu, tunaweka ahadi kwamba tutailipiza kisasi, damu safi ya Imam Shahidi na mashahidi wote wa vita hivi viwili kutoka kwa wauaji wahalifu. Tunawaomba viongozi wa nchi, vikosi vya jeshi, Mashia wote, Waislamu wote na wapenda uhuru duniani wasimame kwa dhati ili kutekeleza madai haya ya haki ya Umma wa Kiislamu. Kwa hiyo, ni lazima viongozi wote wa mfumo wa Kiislamu, taasisi za dola, taasisi za kijamii, wanazuoni, wanafunzi wa Hawza, wabebaji wa ujumbe wa dini, makundi yote ya wananchi, pamoja na mashujaa na watu wenye heshima duniani waitikie wito huu muhimu na waandae mazingira yanayohitajika kwa ajili ya kuutekeleza.

Ujumbe wa Kuendeleza Jihadi na Muqawama na Kurejea katika Msimamo wa Kimsingi wa Uongozi/ Makubaliano Yamekwisha

Ujumbe wa wazi na wa moja kwa moja wa wananchi kupitia ushiriki wao wa kishujaa ulikuwa ni kudai kuendelea kwa jihadi na Muqawama, pamoja na kurejea katika msimamo wa kimsingi wa uongozi.

Sasa kwa kuwa adui, kupitia vitisho, matusi, mashambulizi ya kijeshi, kuendelea kwa vikwazo vya kiuchumi, kutolipa fidia, kutorejesha mali za taifa, kutotekeleza usitishaji vita na kutorudi nyuma kwa Israel wavamizi kutoka ardhi ya Lebanon, na baadaye kurejesha mzingiro wa baharini dhidi ya Iran, amevunja vipengele vyote vya makubaliano hayo; na sasa kwa kuwa Rais wa Marekani ametangaza waziwazi na kwa jeuri kabisa kumalizika kwa makubaliano hayo na kuanzisha vita, basi hakuna tena msingi wa kushikamana na makubaliano hayo wala kuendelea na mazungumzo.

Mheshimiwa Rais mwenyewe, ambaye kwa niaba ya wajumbe wa Shaa amejifunga mbele ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na mbele ya taifa shupavu na lenye msimamo la Iran kutekeleza vipengele vya makubaliano hayo na kusimama dhidi ya tamaa za Marekani, pamoja na wajumbe wengine wa Shaam, makamanda na viongozi wa diplomasia ya nchi, wanapaswa kuyahesabu makubaliano hayo kuwa yamekwisha, wachukue njia ya jihadi na kusimama imara, na kwa utiifu kamili kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu warejee katika njia ile ambayo yeye ameitambua kuwa sahihi.

Taifa Kubwa la Iran Halitatoa Hongo kwa Adui/ Msiendelee na Njia ya Mazungumzo kwa Hofu ya Gharama za Vita

Viongozi waheshimiwa wanapaswa kutambua kwamba; wananchi wale wale wanaobeba mzigo wa matatizo ya kiuchumi yaliyosababishwa na vita pamoja na ukosefu wa busara wa baadhi ya viongozi wa uchumi, ndio haohao wanaotoa madai haya.

Hii ina maana kwamba taifa kubwa la Iran haliko tayari kutoa hongo kwa adui kwa sababu ya matatizo ya kiuchumi, bali liko tayari kujitolea hadi tone la mwisho la damu yake kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kudhihiri Imam Mahdi (as) na kufikia kilele cha ushindi.

Kwa hiyo, viongozi hawapaswi, kwa kisingizio cha matatizo ya kiuchumi, hofu ya gharama za vita, kushambuliwa kwa miundombinu na sababu nyinginezo, kuachana na haki halali za Umma wa Kiislamu wala kuendelea zaidi na njia ya mazungumzo na makubaliano na makafiri ambao, kwa mujibu wa Qur'ani Tukufu, hawashikamani na ahadi yoyote (لَا أَيْمَانَ لَهُمْ).

Badala yake, wanapaswa kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu Muweza wa yote, na kwa kuwa na yakini kamili juu ya sunnah na ahadi za Mwenyezi Mungu zilizotajwa katika aya kama:

«يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنْ تَنْصُرُوا اللَّهَ يَنْصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ»
 (Muhammad: 7),

«قَاتِلُوهُمْ يُعَذِّبْهُمُ اللَّهُ بِأَيْدِيكُمْ وَيُخْزِهِمْ وَيَنْصُرْكُمْ عَلَيْهِمْ وَيَشْفِ صُدُورَ قَوْمٍ مُؤْمِنِينَ»
 (At-Tawbah: 14),

«كَمْ مِنْ فِئَةٍ قَلِيلَةٍ غَلَبَتْ فِئَةً كَثِيرَةً بِإِذْنِ اللَّهِ وَاللَّهُ مَعَ الصَّابِرِينَ»
 (Al-Baqarah: 249),

pamoja na aya nyingine kama 30 ya Suratul Fussilat, 13 ya Suratul Ahqaf, 16 ya Suratul Jinn, 160 ya Suratu Aal Imran na aya nyingine nyingi; na pia kwa kutegemea uungaji mkono wa taifa hili la Waumini, wanamapinduzi, wenye basira, wenye kushikamana na Wilaya, wenye kujitolea na wenye msimamo, waendelee na jihadi kutoka katika msimamo wa nguvu hadi adui ashindwe kabisa, na mpaka kisasi kichukuliwe, fidia ilipwe, mali za taifa zilizozuiliwa zirejeshwe, haki ya Iran ya kusimamia kikamilifu Mlango-Bahari wa Hormuz itambuliwe, pamoja na kutekelezwa kwa masharti mengine yaliyowekwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Ujumbe wa Umoja na Ukuu wa Mhimili wa Muqawama na Ulimwengu wa Kiislamu

Katika mazishi haya ilidhihirika kwamba licha ya mashambulizi makubwa na uovu wa adui Mmarekani na Mzayuni katika kipindi cha miaka miwili au mitatu iliyopita, uhai na ustawi wa Mhimili wa Muqawama umeendelea kwa nguvu zaidi kuliko hapo awali. Mhimili wa Muqawama haujadhoofika; badala yake, matawi yake mapya yamejitokeza wazi, na ndani yake kumeundwa mnyororo wenye nguvu zaidi kuliko ule wa miaka miwili iliyopita.

Ujumbe wa umoja na kuwa mkono mmoja wa Mhimili wa Muqawama mbele ya ukafiri na ubeberu ulikuwa miongoni mwa ujumbe muhimu zaidi wa mazishi haya makubwa.

Ushiriki wa idadi kubwa ya viongozi na wananchi kutoka Iraq, Lebanon, Syria, Yemen na nchi nyingine za Kiislamu katika mazishi yaliyofanyika Tehran, Qom na Mashhad, pamoja na mazishi makubwa na ya kushangaza ya mwili mtukufu wa Imam Shahidi na familia yake yaliyofanyika Najaf na Karbala, na pia uwepo mkubwa wa waombolezaji wa Iraq pamoja na ushiriki wa viongozi na wananchi wengi kutoka Iraq, Lebanon, Yemen na Syria katika hafla hizo, uliutangaza kwa ulimwengu ujumbe wa umoja wa Mhimili wa Muqawama.

Mazishi haya yalionesha mshikamano wa nyoyo za mataifa yote ya Kiislamu na kwamba nyoyo za watu wote wenye heshima na wapiganaji wa njia ya Mwenyezi Mungu katika ulimwengu wa Kiislamu zimeelekezwa kwenye lengo moja, bila kujali mipaka ya kijiografia. Kwa hakika, hili lilikuwa ni ukurasa mpya wa utambulisho mmoja wa Umma wa Kiislamu duniani.

Aidha, utoaji wa heshima na viongozi wa nchi za Kiislamu zisizo na uhasama kwa miili mitakatifu ya mashahidi hawa, pamoja na kufanyika kwa mazishi ya mfano na majlisi za maombolezo katika nchi nyingi za Kiislamu, kulionesha sura ya umoja wa ulimwengu wa Kiislamu na kuthibitisha nafasi ya kimataifa na ya kuvuka mipaka ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu miongoni mwa Waislamu.

Moja ya ujumbe muhimu wa mazishi haya ni kwamba adui mbeberu wa Marekani na Mzayuni ametambua kuwa, licha ya mipango mikubwa aliyokuwa ameandaa dhidi ya taifa la Iran, na licha ya ndoto zake zilizochanganyikiwa za kuuangusha Mfumo wa Kiislamu, mipango hiyo yote imepata fedheha na kushindwa vibaya kutokana na msimamo thabiti wa uongozi, taifa jasiri la Iran na vikosi vya kijeshi vyenye nguvu na ushujaa vya nchi hiyo.

Marekani na Israel, mbele ya utukufu na ukubwa wa taifa la Iran, zimeingia katika mkondo wa kudhoofika na kuelekea kuangamia. Si muda mrefu Marekani italazimika kuondoa uwepo wake katika eneo hili, na Asia Magharibi itasafishwa kutokana na uwepo wao. Kwa upande mwingine, serikali za eneo hili pia hivi karibuni zitatambua kwamba hazipaswi kamwe kuiogopa Marekani, na kwamba kuitumikia Marekani na kumtegemea shetani hakujawahi kuwaletea manufaa wala maslahi yoyote. Hazitakuwa na njia nyingine isipokuwa kukata utegemezi wao kwa Marekani na Israel aliyelaaniwa.

Mwishoni napenda kukumbusha mambo matatu muhimu:

A) Ni muhimu uwepo wa wananchi mitaani uendelee kwa hamasa na utambuzi mkubwa zaidi kuliko hapo awali, na usikatishwe hadi pale Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu atakapotoa maelekezo ya kufanya hivyo.

Viongozi waheshimiwa pia wanapaswa kuweka mazingira bora zaidi ya kuwezesha uwepo huu wa wananchi, wakitambua kwamba uwepo huu ni nguzo ya kuviunga mkono vikosi vya kijeshi katika uwanja wa vita, viongozi wa nchi katika uwanja wa kuwahudumia wananchi, na viongozi wa diplomasia katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha, uwepo huu unafungua njia ya kueneza hukumu na maadili ya Kiislamu, kuyaimarisha ndani ya nyoyo za wananchi, na kuandaa mazingira ya ushiriki mpana zaidi wa wananchi katika kutatua matatizo ya kiuchumi na kitamaduni ya nchi, pamoja na kufanikisha demokrasia ya kidini kwa maana yake halisi.

Ni muhimu kutambua kwamba mwamko mkubwa wa taifa la Iran katika kipindi hiki cha karibuni ni mfano dhahiri wa utukufu, fahari na adhama ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran. Katika ujumbe wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu uliotolewa kwa mnasaba wa mazishi na maziko ya Imam Shahidi, pamoja na kuashiria mwamko huu wa wananchi, alieleza pia chimbuko lake. Kwa mujibu wa kauli yake, Ashura ya Imam Hussein (as) ni mwangwi na mwendelezo wa wito wa Mtume (saww) katika kina cha historia ya mwanadamu; kutokana na mwangwi huo ndipo Mapinduzi ya Kiislamu yalizaliwa, na kutokana na mwangwi huohuo ndipo mwamko wa wananchi ulitokea. Athari na vipengele vya mwamko huu wa wananchi vitakuwa dhamana ya kuufikisha Mfumo wa Kiislamu kwenye malengo na matarajio yake makubwa, Inshaallah.

B) Kulinda umoja na mshikamano wa kitaifa kwa kuzingatia haki na utiifu kwa Walii wa Amri, hususan katika mazingira haya magumu ya vita mseto, ni miongoni mwa wajibu muhimu zaidi. Viongozi, makundi mbalimbali ya wananchi na wanazuoni wa dini wanapaswa, kwa utiifu kamili kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, kuilinda neema hii isiyo na kifani kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kujiepusha na kauli, vitendo au maandishi yoyote yanayoweza kudhoofisha mshikamano huu.

Bila shaka, kulinda umoja na mshikamano wa kitaifa kwa msingi huu hakumaanishi kunyamazia makosa ya kimahesabu au ya kiutendaji yanayofanywa na viongozi. Kinyume chake, kuwakosoa viongozi na kudai haki kutoka kwao, mradi tu kusiambatane na tuhuma, dharau au kuwavunjia heshima, kunasaidia kuimarisha umoja na mshikamano huu.

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwamba viongozi wetu, kama alivyosema Kiongozi wetu mpendwa katika ujumbe wake kuhusu makubaliano, wanafanya juhudi kwa nia njema na kwa uchungu kwa ajili ya taifa. Inshaallah, kutokana na uzoefu walioupata kupitia mazungumzo na makubaliano hayo, watarekebisha makosa yao ya kimahesabu kwa kuongeza utiifu wao kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na kutekeleza ahadi waliyoitoa kwa uongozi na kwa wananchi.

C) Viongozi wote na wenye jukumu la kufanya maamuzi katika Mfumo wa Kiislamu wanapaswa kutumia fursa hii kubwa iliyojitokeza katika vita vya tatu vya kulazimishwa, ili kujenga upya mfumo wa nchi na dola kwa kuzingatia mantiki madhubuti ya Uislamu, maelekezo ya Marajii Wakuu wa Taqlid, misingi, kanuni na fikra za Maimamu wawili wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na mwongozo wa Kiongozi Muadhamu Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei (Mwenyezi Mungu amhifadhi), na pia kwa kutegemea utamaduni wa Muqawama, kusimama imara na busara ya kimapinduzi, ili kufunga njia kwa kila njama na hila za adui mbeberu.

Mwishoni, kwa mara nyingine tena ninatoa mkono wa pole kwa Imam wa Zama, Imam Mahdi (aj), na kwa Naibu wake wa haki, Kiongozi wetu mpendwa, mvumilivu na shujaa, Ayatullah Sayyid Mujtaba Husseini Khamenei, kufuatia shahada ya Imam Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, familia yake na mashahidi wa vita viwili vya karibuni vya kulazimishwa.

Kwa niaba ya wanazuoni wote wa kimapinduzi na wenye kujitolea, tunaweka ahadi pamoja naye na pamoja na taifa jasiri la Iran kwamba tutatoa maisha yetu, mali zetu na heshima yetu katika njia ya Imam Shahidi wetu hadi kufikia kilele cha kudhihiri kwa Imam Mahdi (as).

«وَمَا النَّصْرُ إِلَّا مِنْ عِندِ اللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ»

Alireza A'rafi
Mkurugenzi wa Hawza nchini Iran

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha