Jumamosi 4 Julai 2026 - 10:20
Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ni Uwekezaji wa Kimkakati kwa Mustakabali

Hawza / Khatibu wa Swala ya Ijumaa mjini Qom amesema: Shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ni uwekezaji wa kimkakati kwa ajili ya mustakabali na ni chanzo cha nishati kwa harakati za mapambano na muqawama. Hii ni safari ya milele inayomwambia adui kwamba mlitaka kumwondoa, lakini kupitia safari hii ameenea katika ardhi zote za Kiislamu na amegeuka kuwa fikra isiyoweza kushindwa.

Kwa mujibu wa mwandishi wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Sayyid Muhammad Saeedi alisema katika hotuba za Swala ya Ijumaa ya tarehe 12 Tir 1405 (3 July 2026), iliyofanyika katika Mswala wa Quds mjini Qom, kwamba: Shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi pamoja na familia yake si uhamisho wa mwili kutoka sehemu moja kwenda nyingine tu, bali ni ramani ya njia ya kiroho.

Khatibu wa Swala ya Ijumaa wa Qom aliendelea kusema: Mwanzo wa shughuli za kuaga mjini Tehran una ujumbe kwa viongozi na wananchi, kuaga mjini Tehran kunamaanisha kwamba; Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi alikuwa pamoja na wananchi katika shida na changamoto zao zote, shughuli hizo mjini Tehran ni upya wa kiapo cha utii cha wananchi kwa njia na mwenendo wake pamoja na uongozi wa tatu wa Mapinduzi, wa Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, ili kuwafahamisha maadui kwamba kumuua mtu mmoja hakuwezi kuua malengo na misingi ya mapinduzi.

Aliongeza: Shughuli hizo mjini Qom ni kuunganika na Haram ya Ahlul-Bayt (as), kizazi cha Mtume Muhammad (saww), kuzuru Haram ya Bibi Maasumah (as) na kuunganika na Msikiti wa Jamkaran, haya yote yanamaanisha kurejea kwenye mizizi ya kiroho ya Mapinduzi na chimbuko la Mapinduzi ya Kiislamu, kuletwa kwa mwili wake mjini Qom ni kutembelea watu ambao kila mwaka katika tarehe 19 Dey walikuwa wakimtembelea yeye.

Imamu wa Swala ya Ijumaa wa Qom alisema: Mazishi ya Imam Shahidi mjini Qom yanaonesha umuhimu wa medani ya elimu, jihadi na muqawama, na yanabainisha kwamba elimu bila vitendo na bila shahada haijakamilika, kama alivyotuonesha Imam Hussein (as) kupitia njia hiyo hiyo.

Alisema: Shughuli hizo nchini Iraq pia zinapanua tukio hili kutoka kiwango cha kitaifa hadi kiwango cha Umma mzima wa Kiislamu, kwa sababu Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi alikuwa Imam wa Umma, hapa ndipo ulipo msingi wa uhusiano kati ya shule za Wilayah nchini Iran na maeneo matakatifu ya Wilayah na Uimamu nchini Iraq. Ujumbe wa mazishi haya ni kwamba mhimili wa Muqawama si mhimili wa kijiografia, bali ni mhimili wa kiimani unaounganisha Tehran na Qom, Najaf na Karbala hadi Mashhad, bila kukatika.

Khatibu wa Swala ya Ijumaa wa Qom alisema: Mazishi mjini Mashhad ni kurejea katika kumbatio la Imam wa Nane (as). Kwa mtazamo wa nje, kufika Mashhad kunaonekana kuwa mwisho wa safari, lakini kwa hakika hapo ndipo mwanzo wake. Kuzikwa katika Haram ya Imam Ridha (as) ni alama ya kumzuru Imam Ridha (as) na kukimbilia kwenye hifadhi iliyo salama zaidi kwa Umma.

Aliongeza kuwa Imam Ridha (as) amesema:

«من زارنی علی بُعد داری أتیتُه یومَ القیامة فی ثلاث مواطن حتی اخلّصه من أهوالها: اذا تطایرت الکتب یمیناً و شمالاً و عند الصراط و عند المیزان؛ هر کس مزار مرا با وجود دوریِ راه زیارت کند، در روز قیامت در سه مرحله به عنوان پاسخ زیارتِ او به فریاد وی رسیده و او را از اهوال و دشواری‌های آن مواطن نجات می‌دهم: هنگام تطائر نامه‌های اعمال، وقت عبور از صراط و هنگام بازرسی اعمال»

"Yeyote atakayenizuru licha ya umbali wa safari, nitamjia Siku ya Kiyama katika sehemu tatu ili nimwokoe kutokana na hofu na mashaka yake: wakati vitabu vya matendo vitakaporushwa kulia na kushoto, wakati wa kuvuka Sirat, na wakati wa kupimwa matendo."

Msimamizi wa Haram ya Bibi Maasumah (as) alikumbusha kwamba; jambo la kishujaa katika shughuli hizi ni kuandamana na wanafamilia wake katika mazishi hayo, jambo ambalo linayabadilisha kutoka kuwa tukio la mauaji ya kisiasa na kuwa hamasa ya Hussein. Kwa sababu Imam Hussein (as) pia hakuwepo peke yake Karbala, bali hata mtoto wake mchanga anayenyonya alikuwa pamoja naye.

Aliendelea kusema: Shahada ya familia ya Imam wa Umma ni marudio ya kujitolea kwa Ashura, na inawapelekea maadui ujumbe kwamba; pale ambapo kiongozi anaitoa familia yake yote katika njia ya lengo lake, basi uongozi katika Uislamu si mpango wa kutafuta madaraka bali ni mapenzi ya kuifikia haki, Kiwango hiki cha kujitolea kinaondoa shaka yoyote katika nyoyo za wafuasi.

Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi mjini Qom alisisitiza: Mazishi ya Imam Shahidi ni uwekezaji wa kimkakati kwa ajili ya mustakabali na ni chanzo cha nishati kwa muqawama. Hii ni safari ya milele inayomwambia adui kwamba mlitaka kumwondoa, lakini kupitia safari hii ameenea katika ardhi zote za Kiislamu na amegeuka kuwa fikra isiyoweza kushindwa.

Akirejelea shambulio la meli za kivita za Marekani dhidi ya ndege ya abiria ya Iran mwaka 1367 Hijria Shamsia, lililosababisha kuuawa kishahidi kwa zaidi ya watu 290, pamoja na kukumbusha kugunduliwa kwa njama ya mapinduzi ya Marekani katika Kituo cha Anga cha Nojeh, alisema: Leo, kwa kuzingatia historia hii ya Marekani, tunapaswa kuwa na mtazamo gani kuhusu nchi hiyo?

Imamu wa Swala ya Ijumaa wa Qom aliendelea kusema: Trump muovu, kupitia mpango wa makubaliano, ahadi zisizo na msingi na kununua muda, alitaka kuhakikisha kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz unabaki wazi ili kabla ya uchaguzi wa Marekani utakaofanyika mwezi Aban, bei za mafuta na petroli zishuke, kisha baada ya uchaguzi avunje meza ya mazungumzo na kuishambulia Iran. Jamhuri ya Kiislamu, kwa kutokuwa na imani na ahadi za Marekani, iliugeuza mpango wa makubaliano na mazungumzo kuwa fursa ya kujijenga upya na kuimarisha uwezo wake wa kujihami, na sasa ipo katika kiwango cha juu kabisa cha utayari.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha