Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, matembezi hayo yaliyofanyika jana tarehe 28 Swafar 1448, yaliwakutanisha waumini katika mazingira yaliyojaa hisia nzito, ambapo washiriki walitafakari maisha ya Mtume (saww), juhudi zake za kuufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na nafasi yake kubwa katika kuujenga Umma wa Kiislamu. Kumbukizi hiyo iliwapa waumini fursa ya kurejea katika mafundisho yake na kutafakari wajibu wao wa kuyaendeleza katika jamii.
Tukio hilo liliongozwa na Hujjatul Islaam Sheikh Mwarizo, ambaye alishiriki pamoja na waumini katika matembezi hayo ya amani. Uongozi wake uliambatana na hali ya unyenyekevu na huzuni, huku washiriki wakionesha mshikamano wao katika kuenzi kumbukumbu ya Mtume Muhammad (saww).
Matembezi hayo yalikuwa nafasi ya kuimarisha mshikamano miongoni mwa waumini wa Kishia jijini Tanga na kuonesha kwamba mapenzi kwa Mtume (saww) yanaendelea kuwa sehemu muhimu ya maisha yao ya kiroho. Kwa pamoja, walitembea wakiwa wamebeba ujumbe wa amani, upendo na kuhifadhi mafundisho ya Mtume (saww).








Maoni yako