Jumamosi 4 Julai 2026 - 13:20
Mwili Mtukufu wa Imam Shahidi Utaswaliwa katika Msikiti wa Jamkaran

Hawza/ Msimamizi wa Haram Tukufu ya Msikiti wa Jamkaran ametangaza kwamba: Nyumba Tukufu ya Kiongozi na Ofisi ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu imesisitiza kuwa Imam Shahidi aswaliwe katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran. Kwa msingi huo, kupitia juhudi za usiku na mchana za wahudumu wa Haram hii Tukufu, maandalizi ya tukio hili muhimu la kiroho na la kihistoria sasa yamekamilika.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Ali Akbar Ajaq-Nejad alisema hayo katika kikao cha Kamati ya Maandalizi ya Mazishi ya Mwili Mtukufu wa Kiongozi Shahidi, kilichohudhuriwa na mwakilishi wa Ofisi ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Gavana wa Mkoa, Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Mkoa, Kamanda wa Polisi wa Kitaifa na kundi la viongozi wa mkoa, kilichofanyika katika Haram Tukufu ya Msikiti wa Jamkaran.

Alisisitiza kwamba; Nyumba Tukufu ya Kiongozi na Ofisi ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu imesisitiza kwamba; Swala ya Maiti iswaliwe katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran. Kwa sababu hiyo, kupitia juhudi za usiku na mchana za wahudumu wa Haram hii Tukufu, maandalizi ya tukio hili muhimu la kiroho na la kihistoria sasa yamekamilika. Aidha, aliwataka viongozi kuongeza juhudi zao ili kurahisisha ushiriki mpana zaidi na wa kihistoria wa wananchi katika hafla hiyo.

Msimamizi wa Haram Tukufu ya Msikiti wa Jamkaran aliendelea kusema: Kwa kuzingatia msisitizo wa Nyumba Tukufu ya Kiongozi Shahidi, viongozi husika wanapaswa, pamoja na kuandaa mazingira ya kuswaliwa kwa Swala ya Maiti yenye hadhi kubwa na ya kihistoria juu ya mwili wa Imam Shahidi, pia kuchukua hatua zote muhimu kwa ajili ya maandamano ya mazishi ya mwili wake mtukufu yatakayohudhuriwa na mamilioni ya wananchi wapendwa na wa kimapinduzi wa mji mtukufu wa Qom.

Pia alisema: Matakwa na msisitizo wa wote ni kuhakikisha kuwa mazingira yanaandaliwa ili wananchi wengi zaidi wapate fursa ya kumsindikiza Kiongozi wao Shahidi katika mji mtukufu wa Qom. Tunasisitiza jambo hili, na matarajio yetu kwa viongozi ni kwamba kila sehemu itakayowezekana kufanyika maandamano ya kuusindikiza mwili wa mashahidi, shughuli hizo ziendelee kwa ushiriki wa wananchi.

Mwishoni, Msimamizi wa Haram Tukufu ya Msikiti wa Jamkaran alisema: Ninatumaini kwamba, kwa uwepo wa Marajii Wakuu wa Taqlid, walimu wa Hawza, maulamaa, wasomi, watu wenye elimu na hadhi, wageni wa ndani na wa kimataifa pamoja na makundi yote ya wananchi, Qom utashuhudia shughuli ya kihistoria ya kuuaga mwili wa Imam Shahidi kwa namna bora zaidi.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha