Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Majlisi hiyo iliongozwa na Sheikh Jamali Kasole, ambaye aliwasilisha muhadhara ulioangazia nafasi ya mapambano ya Imam Hussein (as) katika kulinda dini ya Kiislamu na kusimama dhidi ya dhulma na uonevu, aidha, aliwahimiza waumini kuendelea kufuata maadili, subira na kujitolea mambo ambayo yalivyodhihirishwa na Imam Hussein (as) katika tukio la Karbala.
Mamia ya waumini wakiwemo wanawake, wanaume na vijana, walihudhuria maadhimisho hayo yaliyofanyika katika mazingira ya huzuni na majonzi makubwa. Washiriki walishiriki katika usomaji wa Qur'ani Tukufu, nauha na nyimbo za maombolezo, pamoja na dua na kumbukumbu za msiba wa Karbala.
Katika hotuba yake, Sheikh Jamali Kasole alieleza kuwa; Ashura si tukio la kihistoria pekee, bali ni shule ya kudumu inayofundisha kusimama upande wa haki, kupinga dhulma na kujitolea kwa ajili ya kulinda misingi ya dini na utu wa mwanadamu.
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |





Maoni yako