Kwa mujibu wa ripoti ya Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, katikati ya mji wa Iğdır, kundi la wapenzi wa mhimili wa muqawama walikusanyika katika njia ya “Vali Yolu” iliyopo katika kitongoji cha Topçular, na kwa kuunda msafara uliokuwa na takribani magari 500, walifanya maandamano yaliyoashiria kuiunga mkono Iran na Lebanon.
Magari haya ambayo yalipambwa kwa bendera za Uturuki, Iran na Palestina, baada ya kuzunguka katika maeneo ya mji na kupaza sauti za kauli mbiu za kuyaunga mkono mataifa yaliyodhulumiwa, walielekea upande wa mpakani.
Mwanzoni mwa tukio hili, “Wali Badr”, rais wa heshima wa Chama cha Wanazuoni wa Ahlul-Bayt, huku akisisitiza msimamo wa kibinadamu wa watu wa eneo hilo, alisema: Lengo la hatua hii ni kuonesha kwa vitendo na kwa uwazi uungaji mkono kwa Iran na Lebanon, na sisi daima tutasimama dhidi ya dhulma.
Aliongeza: Msafara huu umeundwa kwa ajili ya kufikisha ujumbe huu kwamba mataifa yaliyodhulumiwa hayako peke yao.

Maoni yako