Jumapili 12 Aprili 2026 - 17:30
Hafla ya kumbukumbu ya Arubaini ya kiongozi shahidi yafanyika katika mji mkuu wa Indonesia

Hawza/ Hafla ya kumbukumbu ya siku ya arubaini tangia shahada ya “Ayatullah Sayyid Ali Khamenei”, kiongozi mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ilifanyika katika Husseinia ya “Imamu Khomeini (rh)” ya ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huko Jakarta, kwa kuhudhuriwa na idadi kubwa ya Wairani wanaoishi Indonesia.

Kwa mujibu wa mwandishi wa Shirika la Habari la Hawza, katika hafla hiyo iliyoandaliwa kwa juhudi za Ubalozi wa Utamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Indonesia, Wairani wanaoishi Indonesia kwa kufanya maombolezo na kusoma kwa pamoja Ziara ya Aal Yasin, kwa ajili ya kumbukumbu ya kiongozi shahidi na watoto mashahidi wa shule ya Shajarah Tayyibah Minab, walifanya upya kiapo cha utii kwa malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu.

Katika mwendelezo wa hafla hiyo, Muhammad Boroujerdi, balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Indonesia, kwa kufafanua juhudi na ushujaa wa taifa tukufu la Iran pamoja na wanajeshi wa kujitolea wa nchi hiyo katika vita vya siku arubaini, aliendeleza kumbukumbu na kuhuisha majina ya mashahidi wa Iran na kiongozi shahidi.

Mshauri wa utamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Indonesia pia, kwa kuelezea mitazamo ya kiongozi shahidi na baadhi ya kumbukumbu zake, alitoa heshima kwa nafasi ya juu ya kiongozi huyo shahidi.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha