Jumatatu 6 Aprili 2026 - 15:40
Ayatollah al-‘Udhma Nouri Hamedani awashukuru wananchi wa Iran na vikosi vya ulinzi/ Msirudi nyuma hadi Marekani na utawala wa Kizayuni utakapo shindwa

Hawza/ Mimi, kama mwanafunzi wa Hawza ya Qom, natoa shukrani kutokama na uwepo wenu na uelewa wa hali ya juu, enyi wananchi wapenzi wa Iran, ninawaomba muendelee kudumisha uwepo huu hadi fitna ya Kimarekani na Kizayuni itakapoondoka. Vilevile, muviunge mkono vikosi vya ulinzi, viongozi wa nchi, hususan mihimili mitatu ya dola, na hasa serikali pamoja na Rais, ambao wanaendelea kuhudumu usiku na mchana.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, maandishi kamili ya ujumbe wa shukrani wa Ayatollah Hossein Nouri Hamedani kwa wananchi wapenzi wa Iran, viongozi na hasa vikosi vya ulinzi ni kama ifuatavyo:

بسم الله الرحمن الرحیم

Enyi wananchi wapenzi wa Iran

Katika siku hizi ambazo maadui wa taifa la Iran wameingia katika vita vya wazi kwa kutumia nguvu zao zote, ninyi kwa mwanga wa kipekee mmeandika jina lenu kama mojawapo ya umma bora kabisa, na mmeifanya dhahiri kauli ya Imam marehemu mtukufu aliyesema: «Watu wetu ni bora kuliko watu wa zama za mwanzo wa Uislamu», na pia mmetimiza wazi bishara ya kiongozi shahidi kuhusu kuinuliwa kwenu enyi wananchi.

Leo, watoto wenu walioko katika vikosi vya ulinzi wameweza, kutoksns na umoja wenu na msaada wenu wa pamoja kwa Kiongozi Mkuu “Mola amuhifadhi”, kumlazimisha adui apige magoti, kuvunja ule utukufu wa uongo wa Marekani mhalifu, na kumdhalilisha adui Mzayuni.

Tambueni kwamba yeyote atakayelenga umoja wenu huu, kwa makusudi au bila kukusudia, yuko katika uwanja wa adui.

Mimi, kama mwanafunzi Hawza ya Qom, natoa shukrani kwa uwepo wenu wa uelewa wa hali ya juu, enyi wananchi wapenzi, na ninawaomba muendelee kudumisha uwepo huu hadi fitna hii ya Kimarekani na Kizayuni itakapoondoka; pia muviunge mkono vikosi vya ulinzi na viongozi wa nchi, hususan mihimili mitatu ya dola, na hasa serikali na Rais mheshimiwa ambao wanahudumu usiku na mchana.

Nina neno kwa vikosi vya ulinzi wakiwemo jeshi na Sepah wapendwa, hususan kikosi cha anga na anga-za-nje: Taifa hili lipo pamoja nanyi, na uwepo huu ni kwa ajili ya kuwashukuru na kuwaunga mkono; nami pia ikiwa nina uwezo huo, nitawaombea daima. Ninamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mola wetu wote, Imam al-Mahdi (as) awape ushindi wa mwisho, na ninawaomba ninyi wapendwa katika maeneo matakatifu zaidi—yaani medani ya jihadi—kwa unyenyekevu muniombee dua ya kheri.

Hussein Nouri Hamedani

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha