Jumamosi 14 Februari 2026 - 00:30
Rais wa Pakistan atoa ujumbe wa pongezi kutokana na maadhimisho ya miaka arobaini na saba ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran

Hawza/ Asif Ali Zardari, Rais wa Pakistan, katika ujumbe wake alisisitiza uhusiano wa kihistoria na wa kitamaduni ulio na mizizi ya kina kati ya Tehran na Islamabad, na akatoa pongezi kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka arobaini na saba ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, Rais wa Iran na wananchi wa nchi hiyo. Aidha, alieleza matumaini yake ya kupanuliwa kwa ushirikiano kwa ajili ya uthabiti na ustawi wa eneo zima.

Kwa mujibu wa ripoti ya Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Asif Ali Zardari, Rais wa Pakistan, katika hafla iliyofanyika kutokana na mnasaba wa maadhimisho ya miaka arobaini na saba ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mjini Islamabad, mji mkuu wa Pakistan, alisisitiza kina cha uhusiano kati ya nchi hizo mbili na kusema: Mahusiano kati ya Iran na Pakistan yana mizizi katika historia, lugha, utamaduni na jiografia ya pamoja, na katika miaka iliyopita yameendelea kuimarishwa na kutiwa nguvu zaidi.

Vilevile, alieleza matumaini kwamba roho ya udugu na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili itaendelea kupanuka katika miaka ijayo, na itachukua nafasi yenye athari chanya katika kufanikisha ustawi, uthabiti na mshikamano kwa manufaa ya mataifa yote mawili na eneo zima kwa ujumla.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha