Jumamosi 11 Oktoba 2025 - 22:06
Papa Leo: Waandishi wa Habari wa Ghaza Wako Mstari wa Mbele wa Kuusambaza Ukweli

Hawza/ Papa Leo, katika hotuba yake ya Alhamisi, aliwaheshimu waandishi wa habari mashahidi Ghaza na kusema kwamba; wao wako mstari wa mbele katika kufikisha sauti ya ukweli kutoka maeneo ya vita. Aliwataka waandishi wa habari kuzingatia heshima ya utu wa binadamu na uadilifu katika kazi zao. Papa pia alisisitiza kwamba waandishi wengine wa habari waliotekwa na kushikiliwa na Israel wanapaswa kuachiliwa huru mara moja.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjuma cha Shirika la Habari la Hawza Papa Leo katika hotuba yake ya Alhamisi alieleza umuhimu wa kuchapisha na kusambaza habari sahihi, hasa katika nyakati ambazo watu wengi hujali zaidi umaarufu wa habari kuliko ukweli wake. Avizitaka vyombo vya habari kote duniani kutokusaliti uaminifu wa kusambaza habari za kweli, hasa zile zinazohusu vita.

Papa aliirudia kwa uwazi wito wake wa awali na kusema: “Waandishi wa habari waliotekwa nyara na kuteswa wanapaswa kuachiliwa mara moja; katika sehemu yoyote ya dunia, kazi anayofanya mwandishi wa habari si kosa.”
Akaongeza kuwa: “Hii ni haki ambayo lazima ipiganiwe.” Kisha akawapa heshima maalumu waandishi wa habari mashahidi wa Ghaza.

Kuhusu hali ya sasa ambapo waandishi wa habari wanalazimishwa kubadilisha au kupotosha taarifa chini ya shinikizo, Papa aliieleza hali hiyo kuwa ni batili na isiyokubalika, akisisitiza kwamba uandishi wa habari ni taaluma inayopaswa kila wakati kuongozwa na ujuzi, uadilifu, na ujasiri.

Chanzo: Habari za Vatikani

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha