Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Maulidi ya kitaifa mwaka huu wa 2025 yamenyika Mkoani Tanga, katika wilaya ya Korogwe kwenye viwanja vya Shule ya Mazoezi Manundu usiku wa kuamkia leo, katika Hfla hii viongozi mbali mbali walihudhururia akiwemo Sheikh mkuu wa Jumuiya ya Shia nchini Tanzania (TIC), Samahat Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge akiongozana na ujumbe wake kamili.
vilevile miongoni mwa nyuso za kishia ambazo zilipata bahati ya kuhudhuria kwenye hafla hiyo hiyo, mwakilishi wa chuo cha Jaamiatul-Mustafa, Dkt, Ally Taqawi, ambae nae pia aliongozana na ujumbe wake maalumu, hafla kama hii hufanyika kila mwaka ambapo kwa mujibu wa Riwaya za Ahlu Sunnah sherehe hizi hufanywa tareh 12 mfungo sita, huku riwaya za Ahlulbayt zikwa zimebainisha kwamba tukio hili lilitokea tareh 17 mfungo sita, kutokana na utofauti huu wa riwaya Maulamaa wa kishia huitambua wiki hii nzima kama vile "wiki ya umoja".
Zifuatazo ni picha mbali mbali zinazo akisi mahudhurio ya watu katika hafla hiyo
Maoni yako