Alhamisi 27 Agosti 2026 - 17:51
Ayatullah Al-Udhma Sistani Aanzisha Mpango wa Kuwasaidia Yatima wa Lebanon Walioathiriwa na Vita

Hawzah/ Ofisi ya Ayatullah Sistani nchini Lebanon imetangaza mpango wa kuwasaidia yatima walioathiriwa na vita katika nchi hiyo.

Kwa mujibu wa Idara ya Kimataifa ya Shirika la Habari la Hawza, Ofisi ya Ayatullah Sayyid Ali Sistani nchini Lebanon, kupitia taarifa iliyotoa, imetangaza kuanzishwa mpango mpya wa kibinadamu wa kutoa msaada wa kifedha kwa yatima waliotokana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya nchi hiyo.

Mpango huo unalenga kuwasaidia yatima ambao hawako chini ya uangalizi wa taasisi yoyote au jumuiya ya hisani, kwa kuwapatia msaada wa kifedha wa kila mwezi.

Lengo kuu la mpango huu ni kupunguza maumivu na mateso wanayopitia yatima walioathiriwa na vita nchini Lebanon.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha