Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Madrasa ya Imam Khomeini (rh) mjini Najaf Ashraf, inayosimamiwa na Ofisi ya mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi nchini Iraq, ikiwa na takriban wanafunzi 400 wa kimataifa kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu za eneo hili, inapokea wanafunzi wa Hawza katika ngazi zote za masomo ya hawza kwa kufuata mfumo wa masomo na manhaji ya Hawza ya Najaf; kuanzia ngazi za utangulizi (muqaddamat), kiwango cha kati (sath'h), hadi ngazi za juu za hawza (sutuh al-'ulya).
Wanafunzi wote kwanza hupitia mafunzo ya lugha ya Kiarabu kwa muda wa miezi 3 hadi 6, na baada ya kukamilisha kipindi hicho hupelekwa katika madaraja ya masomo yanayolingana na kiwango chao.
Faida zinazotolewa
Makazi.
Mazingira mazuri ya elimu na ufundishaji.
Maktaba na ukumbi unaofaa wa kujisomea.
Programu za ziada za utafiti, malezi ya kiroho na shughuli za tablighi sambamba na masomo.
Kutengewa hadia ya kila mwezi wakati wa kipindi cha masomo.
Uwezekano wa kulinganisha na kuidhinisha masomo ya madrasa na mfumo wa Hawza za Iran, pamoja na kusajiliwa moja kwa moja kwa alama za masomo ya Najaf katika mfumo wa tathmini ya elimu wa Iran.
Kuendelea kubaki hai kwa jalada la mwanafunzi la masomo.
Muda wa Usajili
Kuanzia tarehe 15 Khordad hadi 15 Tir 1405 Shamsia.
Jinsi ya Kujisajili
Kwa ajili ya usajili, tuma ujumbe wenye neno:
«ثبت نام» (Usajili)
kwenda kwenye namba ya simu tajwa hapa chini au katika tangazo kupitia programu ya mawasiliano ya Baleh.
۰۰۹۶۴۷۷۰۶۳۵۲۵۴۰

Maoni yako