Kwa mujibu wa kitengo cha kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Ibrahim Zakzaky, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria, katika hafla ya kufunga kongamano la vijana la “Sadat” la Harakati ya Kiislamu lililofanyika katika makazi yake mjini Abuja, huku akirejelea fadhila za mwezi wa Dhul-Hijjah, aliuelezea mwezi huu kuwa umejaa matukio muhimu katika historia ya Uislamu.
Katika sehemu ya hotuba yake aligusia ndoa ya Amirul-Muuminina Imam Ali ibn Abi Talib na Fatimah al-Zahra, na akaieleza kuwa ni mfano wa namna sahihi ya ndoa katika Uislamu.
Sheikh Zakzaky pia, akirejelea kisa cha Nabii Ibrahim na utayari wake wa kumtoa mwanawe Nabii Ismail kuwa kichinjwa katika njia ya Mwenyezi Mungu, alisema: Falsafa ya kuchinjwa kwa hakika inaonesha roho ya kujitolea na kujitoa muhanga.
Aliongeza: kichinjwa chetu leo ni kwamba, mwanadamu aazimie kujitolea kila alicho nacho katika njia ya dini ya Mwenyezi Mungu.
Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria aliendelea kwa kusisitiza nafasi ya juu ya Ahlul-Bayt (a.s.) na akasema: Ahlul-Bayt (a.s.) wamechaguliwa kwa hekima ya Mwenyezi Mungu, na kuwafuata wao ni njia ya wokovu.
Akiwaonya kuhusu mizizi ya husuda katika historia alisema: Pale Mwenyezi Mungu anapompa mtu cheo na nafasi fulani, kuipinga hali hiyo kunaweza kumfikisha mwanadamu katika hatima ya Iblisi. Kama ilivyokuwa katika historia ambapo baadhi ya Mayahudi walimhusudu Mtume Muhammad kwa sababu hakutoka kwao; na Iblisi naye aliangamia kwa sababu ya husuda dhidi ya Nabii Adam.
Mwishoni, Sheikh Zakzaky akiwaelekeza vijana, alisisitiza: Mapenzi kwa Ahlul-Bayt (a.s.) si kauli mbiu tu, bali ni jambo ambalo mwanadamu anatakiwa ndani yake kuisalimisha nafsi yake katika njia yao na kwa vitendo kufuata mwenendo wao.
Maoni yako