Jumapili 17 Mei 2026 - 15:00
Tusome Qur’ani | Katika jamii isiyo ya Kiislamu unatamani kuwa mwema, lakini huwezi

Hawza/ Katika jamii isiyo ya Kiislamu, mwanadamu licha ya kuwa na hamu ya mwema na mwenye dini, kutokana na shinikizo la mazingira hawezi kuwa mwenye kushikamana na dini, na sababu zote humweka mbali na kumkumbuka Mwenyezi Mungu; lakini katika jamii ya Kiislamu, soko, msikiti, serikali, familia na marafiki vyote humkumbusha mwanadamu Mwenyezi Mungu, na lau utawala wa Mtume na wa Alawi ungeendelea, baada ya miaka hamsini wanafiki wote wangekuwa Waumini wa kweli.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, katika jamii isiyo ya kimungu, mwanadamu hata akitaka kiasi gani kuwa mwenye dini, mazingira humweka mbali na Mwenyezi Mungu; lakini jamii ya Kiislamu ni kiwanda cha kuwajenga wanadamu ambapo vipengele vyake vyote – kuanzia sokoni hadi katika familia – humkumbusha mwanadamu Mwenyezi Mungu. Lau utawala wa Mtume na wa Alawi ungeendelea, hata wanafiki pia wangekuwa Waumini.

Faili maalumu ya “Tusome Qur’ani” inaelezea tafsiri za Qur’ani kutoka kwa Kiongozi Shahidi, ambapo katika toleo hili tutachunguza mada isemayo: “Jamii ya Kiislamu humkurubisha mwanadamu kwa Mwenyezi Mungu”, ambayo matini yake tunaiwasilisha kwenu kama ifuatavyo:

Katika jamii zisizo za Kiislamu na zisizo za kimungu, watu wanataka kuwa wema lakini hawawezi; unatamani kuwa mwenye dini lakini huwezi, unatamani usitoe riba wala usile riba, lakini unaona haiwezekani.

Mwanamke anatamani asitoke nje ya heshima na usafi wa Kiislamu, lakini mazingira humwekea shinikizo.

Sababu zote na vichocheo vyote humweka mwanadamu mbali na kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Picha, maonyesho, mapambo, matembezi, mahusiano, biashara na mazungumzo, vyote humweka mwanadamu mbali na Mwenyezi Mungu na humfanya ukumbusho wa Mwenyezi Mungu kuwa mgeni ndani ya moyo wake, Katika jamii ya Kiislamu hali ni kinyume chake.

Katika jamii ya Kiislamu, soko lake, msikiti wake, makao ya utawala wake, rafiki yake, ndugu yake, baba wa familia, kijana wa familia, vyote kwa pamoja humkumbusha mwanadamu Mwenyezi Mungu, humvuta kuelekea kwa Mwenyezi Mungu, humfanya apatane na Mwenyezi Mungu, huanzisha uhusiano na Mwenyezi Mungu, humfanya awe mja wa Mwenyezi Mungu na humweka mbali na utumwa wa asiye Mwenyezi Mungu.

Lau jamii ya Kiislamu ya zama za Mtume ingedumu kwa miaka hamsini, uongozi ule ule ungeendelea kubaki madarakani, au baada ya Mtume, Ali bin Abi Twalib (as) kwa uongozi ule ule aliouteua Mtume angekaa mahali pa Mtume, basi hakikisheni jambo hili: baada ya miaka hamsini, wanafiki wote wangekuwa Waumini wa kweli.

Lau wangeacha utawala wa Kinabii na wa Alawi uendelee mmoja baada ya mwingine, jamii hiyo inayojenga wanadamu kwa namna ya lazima ingewatakasa hata watu wote wenye unafiki, ingeifanya mioyo yote yenye unafiki kuwa ya Kiimani, na wale wote ambao roho zao hazikuwa zimezoea imani wangemjua Mwenyezi Mungu na kuwa na imani, hii ndiyo tabia ya jambo linalohusiana na jamii ya Kiislamu.

Mitume huja ili kuanzisha jambo kama hili, hili linapojengwa, kama kiwanda cha kutengeneza wanadamu, si mmoja mmoja, si kumi kumi, si mia mia, bali makundi kwa makundi na misafara kwa misafara, watu wanakuwa Waislamu; Waislamu wa nje katika masuala ya dhahiri ya Kiislamu, na pia Waislamu na Waumini wa moyoni, wa kweli na wa ndani. Je, hili limeeleweka? Basi Mtume huja kwa ajili ya kazi kama hii.

Chanzo: Kitabu “Muhtasari wa Jumla wa Fikra ya Kiislamu ndani ya Qur’ani”, mlango wa Tawhidi, kikao cha 23, ukurasa wa 411.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha