Alhamisi 9 Aprili 2026 - 10:20
Rais wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia Pakistan: Iran imesimama kwa fahari na adui amelazimika kurudi nyuma

Hawza/ Hujjat al-Islam wal-Muslimin Sayyed Sajid Ali Naqvi, katika ujumbe wake akijibu kukubaliwa kwa masharti ya kusitishwa kwa mapigano na upande wa adui alisisitiza kuwa; Iran leo imesimama kwa fahari na Marekani pamoja na Wazayuni wamelazimika kurudi nyuma.

Kwa mujibu wa idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, Sayyed Sajid Ali Naqvi katika ujumbe wake huku akijibu kukubaliwa kwa masharti ya kusitishwa kwa mapigano na upande wa adui alisisitiza kuwa; Iran leo imesimama kwa fahari na Marekani pamoja na Mazayuni wamelazimika kurudi nyuma.

Katika ujumbe huo imeelezwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kutoa sadaka kubwa katika kihistoria, imelinda uhuru, kujitegemea na utambulisho wake wa kitamaduni, na imekuwa sababu ya kuinuliwa kwa heshima katika ulimwengu wa Kiislamu. Vilevile, nafasi ya Pakistan katika uwanja wa diplomasia, ikiwa ni ya vitendo na yenye athari, inastahili kupongezwa.

Aidha, kwa kuashiria kupita kwa siku arobaini tangia mashambulizi na kutangazwa kwa usitishaji wa mapigano wa siku kumi na tano pamoja na kukubaliwa kwa mpango wa vipengele kumi wa Iran, ameongeza kuwa: leo kwa baraka ya damu takatifu ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Mtukufu Ali Khamenei (ra), na kwa uongozi wenye hekima wa Mojtaba Khamenei, pamoja na kujitolea kukubwa kwa taifa la Iran, nchi hii imepata heshima na maadui wamesukumwa nyuma. Mataifa yaliyo hai yako tayari kutoa sadaka kubwa zaidi, lakini kamwe hayafanyi biashara juu ya heshima, uhuru, kujizuia, haki na rasilimali zao. Taifa kubwa la Iran pia kwa mtazamo huu, si tu limelinda uhuru na kujitegemea pamoja na utambulisho wake wa kitamaduni, bali pia kwa kuinua heshima ya ulimwengu wa Kiislamu, limefungua upeo mpya kwa ajili ya amani, uthabiti na ushirikiano wa kikanda.

Rais wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia wa Pakistan amesisitiza kuwa: diplomasia ya Pakistan iliyo makini na yenye ufanisi, mawasiliano endelevu na yenye athari na pande zote kwa ajili ya kufanikisha amani ya kikanda, pamoja na kutekeleza nafasi yake kama nguvu ya nyuklia yenye kuwajibika na inayotafuta amani, ni jambo la kupongezwa; hali ambayo imepelekea kuimarika kwa nafasi ya Pakistan katika ulimwengu wa Kiislamu na hata katika kiwango cha kimataifa.

Mwisho, mwanazuoni huyu mashuhuri wa kidini ameonya kuwa; ukoloni na Uzayuni wanaweza kwa njama mpya kujaribu kudhoofisha mafanikio haya, jambo ambalo linapaswa kufuatiliwa kwa makini.

Amehitimisha kwa kuwatakia pongezi watu wa Iran na Pakistan kwa mafanikio haya, na kuwaombea kheri na mafanikio.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha