Ijumaa 27 Machi 2026 - 08:00
Chama cha Kiislamu cha Mu'talifah Chatuma Ujumbe wa Rambirambi kwa Hashd al‑Shaabi, Iraq

Hawza/ Kitengo cha Kimataifa cha Chama cha Mu'talifah, kimetoa salamu za rambirambi kutokana na shahada ya kundi la wapiganaji wa Hashd al‑Shaabi Iraq, katika shambulio la Wamarekani na Wazayuni.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, kutoka Tehran, Kitengo cha Kimataifa cha Chama cha Mu'talifah ya Kiislamu kimetoa ujumbe wa rambirambi kufuatia shahada ya kundi la wapiganaji wa Hashd al‑Shaabi Iraq katika shambulio la Marekani na Wazayuni.

Katika ujumbe huu, uliowasilishwa kwa Faleh al‑Fayyadh, Katibu Mkuu wa Shirika la Badr na Mkuu wa Baraza la Hashd al‑Shaabi, pamoja na wanachama wa taasisi hii ya mapambano, kumesisitizwa kuwa: “Tena mara nyingine mkono wa jinai wa Marekani na utawala ghaṣibu wa Kizayuni umejaa damu safi ya wapiganaji wanaotafuta haki ndani ya Iraq adhimu. Shambulio hili linaonesha kina cha uovu wa maadui wa pamoja wa Umma wa Kiislamu na mwendelezo wa siasa chafu ya uvamizi na kuchochea kutoendelea kwa amani katika eneo.”

Kitengo cha Kimataifa cha Chama cha Mu'talifah, sambamba na kulaani vikali kitendo hiki cha uvamizi, kimetoa mkono wa rambirambi kutokana na shahada ya wapiganaji mashujaa wa Hashd al‑Shaabi kwa hadhara ya Hadhrat Wali al‑Asr (a.s), Mar'aji wa kidini, serikali na taifa tukufu la Iraq, na hasa kwa familia tukufu za mashahidi na wenzao wa karibu, na kimesisitiza kuwa: “Damu takatifu ya mashahidi hawa wa cheo kikubwa kamwe haitapotea bure, na itaongeza uimara wa mrengo wa mapambano dhidi ya tamaa za ubeberu wa kimataifa.”

Katika sehemu nyingine ya ujumbe huu imeelezwa kuwa: “Sisi katika Chama cha Mu'talifah tunashirikiana nanyi huzuni na heshima yenu, na kwa udugu tunatangaza kuwa katika njia hii yenye heshima kubwa, tutakuwa pamoja nanyi na nyuma ya taifa imara na mpiganaji la Iraq.”

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha