Jumapili 22 Februari 2026 - 10:36
Ayatullah A‘rafi, Katika kikao na wafanya biashara wa Qum, Iran

Hawza/ Akizungumzia umuhimu wa nafasi ya Qum katika historia ya elimu na dini, alisema kuwa Qom tangu zamani imejulikana kama kituo cha kielimu na kidini. Mji huu kwa zaidi ya miaka 1200 umekuwa kitovu cha elimu na dini, na historia hii ina umuhimu mkubwa sana kwetu.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza,  Mjumbe wa wanazuoni wa Baraza la Kulinda Katiba nchini Iran, aliendelea kusema kuwa; hata kabla ya kuzikwa Bibi Fatima Masumeh (amani iwe juu yake) katika mji wa Qom, Qom tayari ilikuwa ikitambulika kama eneo muhimu la kidini na kitamaduni, na hadi leo mji huo ni kitovu cha kueneza utamaduni wa Kiislamu na wa kidini.

Nafasi ya Qom Katika Historia

Mkurugenzi wa Hawza za Elimu ya Kiislamu, alisisitiza umuhimu na mchango wa watu wa Qom katika kuhifadhi na kuendeleza utamaduni huu wa kidini, akiongeza kuwa: Qom katika historia yake haijawahi kupotoka kutoka katika njia ya kielimu na kidini. Wakati miji mingi kama Ray au Baghdad ilitengana na mwelekeo huo kutokana na matukio mbalimbali, Qom imeendelea kusimama imara katika njia hiyo.

Aidha, aligusia nafasi maalumu ya Qom katika historia ya Uislamu na Ushia, akieleza kuwa; katika vipindi mbalimbali vya historia, Qom imekuwa ikitambulika kama kituo muhimu cha kielimu na kidini kwa Waislamu, hususan Mashia. Katika zama tofauti, mji huo haujawahi kukengeuka katika mawasiliano yake ya kielimu na kidini, jambo linaloufanya utambulike na kutofautiana na maeneo mengi mengine.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha