Alhamisi 17 Julai 2025 - 00:15
Mapumziko na matembezi kwa mtazamo wa Imam Khomeini (ra)

Hawza/ Ayatollah Mirza Jawad Agha Tahrani (ra), mmoja wa mauraf'a na miongoni mwa mafaqihi wa Kishia, katika kisa kimoja cha kipindi chake cha masomo katika Hawza ya kielimu ya Qom, alisimulia kuhusiana na masharti mawili muhimu aliyokuwa nayo Imam Khomeini (ra) kwa ajili ya kushiriki katika programu za matembezi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Mirza Jawad Agha Tahrani (ra) katika moja ya kumbukumbu zake anasema: Katika kipindi cha masomo katika Hawza ya kielimu ya Qom, wakati mwingine baadhi ya marafiki wa Haj Agha Ruhullah [Imam Khomeini] walikuwa wakimsisitizia sana ili siku moja ya mapumziko waende matembezini nje ya mji ili apate kupumzika kidogo.

Lakini Agha [Imam] hakuwa anakubali, na nyakati ambapo msisitizo ulikuwa mkubwa mno, alikuwa anakubali kuja lakini kwa masharti mawili:

1. Popote ambapo muda wa swala ungewadia, hata kama ni mahali pasipofaa, swala iswaliwe kwa wakati wake wa mwanzo.

2. Kusiwepo mtu yeyote atakayezungumza jambo ambalo harufu ya kusengenya inaweza kunukia kutoka ndani yake.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha