Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Sayyid Muhammad Saidii, katika khutba za Swala ya Ijumaa ya tarehe 27 Shahrivar 1405 (Sept 18 2026), zilizofanyika katika Muswalla wa Quds Mjini Qum, huku akizungumzia kumbukumbu ya kuanza vita vilivyolazimishwa na utawala wa Baath wa Iraq dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema: Mwaka huu, sambamba na Wiki ya Ulinzi Mtakatifu, tunashuhudia ushindi wa operesheni ya Ansarullah ya Yemen.
Ameendelea kusema: Kukombolewa maelfu ya kilomita za maeneo ya kimkakati ya Yemen kutoka kwa mamluki wa Saudi Arabia, kwa baadhi ya vipengele, kunafanana na ukombozi wa Khorramshahr mwaka 1361, kama ambavyo ukombozi wa Khorramshahr ulibadilisha mizani ya vita vilivyolazimishwa dhidi ya Iran na kuushangaza ulimwengu, hatua za leo za wapiganaji Waislamu nchini Yemen, ambazo zimesababisha kudhibitiwa kwa Mlango-Bahari wa Bab al-Mandab, zimebadilisha pia mizania ya vita dhidi ya Wasaud na zimeushangaza ulimwengu.
Imam wa Swala ya Ijumaa ya Qum ameongeza: Kipengele muhimu zaidi cha operesheni hizi mbili ni imani na itikadi zinazofanana baina ya wapiganaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na wapiganaji Waislamu nchini Yemen.
Amesisitiza kwamba sababu kuu ya ushindi huu ni imani zinazofanana na imani ya wapiganaji Waislamu. Sababu kuu ya ushindi katika operesheni zote mbili ni nusura ya Mwenyezi Mungu. Kama ambavyo jana Mwenyezi Mungu aliikomboa Khorramshahr, leo pia amekomboa Bab al-Mandab na ameipa safu ya Muqawama nafasi mpya katika upande wa nguvu.
Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi Qum ameonya: Madhalimu wa dunia na mamluki wao wa kikanda wanapaswa kujua kwamba njia ya kuongezeka nguvu ya safu ya Uislamu na kusonga mbele hadi kufikia ushindi wa mwisho itaendelea, kwa sababu wapiganaji wa Uislamu, popote walipo, wanaamini kwamba:
«وما النصر الا من عند الله العزیز الحکیم»
“Na ushindi hautoki isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.”
Ameongeza: Sote tunapaswa kuamini ahadi hii ya Mwenyezi Mungu na kuendelea kuwa katika mstari wa mapambano hadi ushindi wa mwisho. Kwa sababu hiyo, kwa zaidi ya nyusiku 200, wananchi wenye kushikamana na Wilaya, wazalendo na wenye imani, wakiwa na imani katika nusura hii ya Mwenyezi Mungu, wameendelea kubaki viwanjani, wakipeperusha bendera zilizoandikwa “یا لثارات الحسین” na “یا لثارات الخامنهای”, pamoja na bendera ya Jamhuri ya Kiislamu, na wakiwa wamekunja ngumi zao wakitaka kulipiza kisasi kutoka kwa adui mhalifu kwa sababu ya kumuua kishahidi Imam wa Umma, makamanda, wanasayansi, abiria wa meli ya Dena na watoto wasio na hatia wa shule ya Minab.
Msimamizi wa Haram Tukufu ya Hadhrat Fatima Ma’suma (sa) ameendelea kusema: Wananchi wetu, kupitia vilio vyao, wanaitumia dunia ujumbe kwamba yeyote anayefikiria kuivamia Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anapaswa kujiandaa kupokea makofi makali na ngumi za chuma.
Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, akizungumzia kuanza kwa mwaka mpya wa masomo, amesema: Imam Ali (as), kuhusu umuhimu wa kusoma katika kipindi cha ujana, amesema: «مَن لَم یَتَعَلَّمْ فی الصِّغَرِ لَم یَتَقَدَّمْ فی الکِبَرِ» — “Mtu ambaye hakujifunza akiwa mdogo hatapiga hatua akiwa mtu mzima.”
Imam wa Swala ya Ijumaa ya Qum, huku akisisitiza kwamba wanafunzi na watoto wadogo walio chini ya uangalizi wa taasisi ya utamaduni ya nchi ni hazina na rasilimali yenye thamani kubwa zaidi na iliyojaa uwezo kwa taifa hili, amewaambia wanafunzi: Someni kwa bidii; mustakabali wa nchi ni wenu.
Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Qum, katika kuendelea kwa hotuba yake, akiheshimu kumbukumbu ya mashahidi wa tukio la Mina, amesema: Usalama wa mahujaji ni miongoni mwa masuala muhimu sana. Tukio la Mina la mwaka 1399 ni jeraha lisilosahaulika katika nyoyo za Umma wa Kiislamu.
Akitoa pongezi kwa kuzaliwa Imam Hasan al-Askari (as), amesema: Kipindi cha maisha yenye baraka na yaliyojaa hatari cha Imam Hasan al-Askari (as) ni hitimisho la mwanadamu mwema wa miaka 250. Mwanadamu ambaye ndani yake alikuwa akifuatilia uwepo wa Maimamu 11 kwa lengo la kuanzisha utawala wa Tawhidi katika jamii za wanadamu na kuunda ustaarabu wa Kiislamu. Imam Hasan al-Askari (as) alijitahidi kutekeleza mfumo mbadala wa muundo wa uongozi wa Maimamu waliokuwepo, ili aweze kujibu mahitaji ya Mashia katika kipindi cha Ghaiba, njia hii iliambatana na uteuzi wa Naibu Maalumu, Manaibu wa Jumla na Wali al-Faqih.
Ameendelea kusema: Kipindi cha Imam Hasan al-Askari (as) kilikuwa na vikwazo vikali na kilikabiliwa na dhuluma za Makhalifa wa Bani Abbas. Pamoja na kwamba Uimamu wake ulikuwa wa miaka sita, matukio muhimu yalitokea katika kipindi hicho, miongoni mwao ikiwa ni kuwaandaa Mashia kwa kipindi cha Ghaiba, kumtambulisha Imam wa mwisho kwa Mashia maalumu, kuzima fitina za kiitikadi na kueneza zaidi na zaidi Madhehebu ya Shia.
Imam wa Swala ya Ijumaa ya Qum, akizungumzia kumbukumbu ya kifo cha Hadhrat Fatima Ma’suma (sa), amesema: Hadhrat Ma’suma, kwa kuingia kwake Qum, alibadilisha jiografia ya kiroho ya Iran. Hadhrat Ma’suma (sa) ni mfano wa hali ya juu kwa mabinti wa Iran katika kulinda usafi wa maadili na haya, pamoja na kujenga ustaarabu. Hazrat Ma’suma (sa) ni mjukuu wa Imam mwenye msimamo wa kimapinduzi, mwanamke wa kiwango cha juu cha Kiislamu, mwenye maisha ya kujisitiri, mwenye kushiriki katika masuala ya jamii na mwenye kuongeza uelewa.
Amesema: Miongoni mwa sifa bora za Hadhrat Ma’suma (sa) ni kwamba Imam Swa'diq (as), miaka mingi kabla ya kuzaliwa kwake, alisema:
«تَدخُلُ بِشَفاعَتِها شِیعَتی الجَنَّةَ بِأجمَعِهِم»
“Mashia wangu wote wataingia Peponi kwa shifaa yake (Fatima Ma’suma, amani iwe juu yake).”
Mwisho mwema wa maisha pia ni miongoni mwa baraka za kumzuru Hadhrat Ma’suma (sa). Imam Jawad (as) amesema kuhusu jambo hili: «مَنْ زارَ قَبْرَ عَمَّتی بِقُمَّ فَلَهُ الْجَنَّةُ» — “Mwenye kuzuru kaburi la shangazi yangu huko Qum, basi atapata Pepo.”
Maoni yako