Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjam cha Shirika la Habari la Hawza, Shura ya Kisiasa ya Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq ilifanya kikao chake cha mara kwa mara katika makao ya Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq, katika Mkoa wa Najaf Tukufu, kwenye ukumbi wa Imam Ali (as), chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mahusiano ya Kisiasa. Kikao hicho kilihudhuriwa na Sanaa Al-Mousawi, mshauri wa Waziri Mkuu kuhusu masuala ya ulinzi wa kijamii, pamoja na maafisa wa ofisi katika kituo, vitengo na maeneo mbalimbali, wajumbe wa Baraza Kuu na Ofisi ya Ujenzi wa Serikali.
Maelekezo ya kimaadili na malezi
Hujjat al-Islam wal-Muslimin Seyyed Sadruddin Qabanji, Imamu wa Swala ya Ijumaa wa Najaf Tukufu na mjumbe wa Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq, alianza kikao hicho kwa hadithi ya kidini na kimalezi, kwa kuzingatia wasia wa Mtume Mtukufu Muhammad (saw) kwa Amir al-Mu’minin Imam Ali (as):
(یا علی، ثلاثة تحت ظل العرش یوم القیامة: رجل أحب لأخیه ما أحب لنفسه ورجل بلغه أمر فلم یقدم فیه ولم یتأخر حتی یعلم أن ذلک الأمر لله رضا أو سخط ورجل لم یعب أخاه بعیب حتی یصلح ذلک العیب عن نفسه فإنه کلما أصلح من نفسه عیباً بدا له منها آخر وکفی بالمرء فی نفسه شغلاً)
“Ewe Ali! Kuna watu watatu watakaokuwa chini ya kivuli cha Arshi Siku ya Kiyama: Mtu anayependa kwa ndugu yake kile anachokipenda mwenyewe; mtu ambaye anapofikishiwa jambo fulani, halikimbilii wala halicheleweshi mpaka ajue ikiwa jambo hilo ni lenye ridhaa ya Mwenyezi Mungu au ghadhabu Yake; na mtu ambaye hamlaumu ndugu yake kwa kosa mpaka kwanza awe amerekebisha kosa hilo ndani yake mwenyewe. Kwa hakika, kila anaporekebisha kosa moja ndani yake, hujidhihirisha kwake kosa jingine, na inamtosha mtu kujishughulisha na makosa yake mwenyewe.”
Alisisitiza umuhimu wa kutekeleza hadithi hii yenye baraka na akasema: “Mikutano na vikao kama hivi vya kirafiki vinaambatana na mapenzi, na vinapata ridhaa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na Ahlul-Bayt (as).”
Hujjat al-Islam wal-Muslimin Seyyed Sadruddin Qabanji alisisitiza umuhimu wa kudhihirisha msingi wa “kujitoa kwa ajili ya wengine (ithaar)” katika mambo ambayo mtu anayapendelea kwa ajili yake mwenyewe, kwa lengo la kuimarisha mshikamano na umoja wa kindugu.
Hali ya ndani: Mabaraza ya mikoa na suala la kuweka silaha chini ya udhibiti
Katika sehemu ya siasa za ndani, Imamu wa Swala ya Ijumaa wa Najaf Tukufu alizungumzia kwa ujumla matukio mbalimbali yanayoendelea nchini Iraq na kuelekeza mkazo kwenye masuala muhimu zaidi yanayojadiliwa katika vikao vya “Mfumo wa Uratibu” (Al-Ittaar Al-Tansiqi) pamoja na taasisi za serikali na utawala.
Hujjat al-Islam wal-Muslimin Qabanji, akirejelea kwamba pendekezo la kuvunjwa kwa mabaraza ya mikoa ni suala linalojadiliwa na kujadiliwa kwa mapana, alieleza: “Kuna mitazamo miwili mikuu: Wa kwanza unataka mabaraza hayo yavunjwe, wakati wa pili unaamini kwamba kuvunjwa kwake si jambo la kisheria isipokuwa kwa kurejea kwenye matakwa ya kisheria yaliyowekwa kwa ajili ya kuyadhibiti.”
Alirejelea mashauriano yaliyofanyika ndani ya “Mfumo wa Uratibu”, yakihudhuriwa na Waziri Mkuu, na akasisitiza kwamba; msimamo thabiti ni kukataa uamuzi wa kukabidhi silaha, isipokuwa baada ya kuondoka kikamilifu kwa majeshi ya muungano unaoongozwa na Marekani nchini Iraq.
Katika ngazi ya kikanda na kimataifa, Imamu wa Swala ya Ijumaa wa Najaf Tukufu alitahadharisha kuhusu matukio hatari ya kiusalama na kisiasa, na akaelezea harakati na dalili zinazohusiana na muungano wa kikanda na kimataifa, pamoja na kufanyika mashambulizi dhidi ya makazi ya Al-Hashd Al-Sha’abi.
Hujjat al-Islam wal-Muslimin Seyyed Sadruddin Qabanji alisema: “Kuna alama kubwa ya swali kuhusu malengo halisi yaliyo nyuma ya mashambulizi haya, na iwapo kwa msingi wake yanalenga kubadilisha mwelekeo wa kisiasa nchini Iraq au la.”
Maoni yako