Jumanne 7 Julai 2026 - 09:09
Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Hawza/ Hatimaye wakati uliokuwa ukisubiriwa wa ziara ya mwisho ya Bwana Shahidi katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran na kukutana kwa Umma wa Kiislamu na kiongozi wao katika mji wa Bibi Mtukufu wa Ahlul-Bayt (Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake) umefika. Hakika nyakati hizi ni za uchungu mkubwa kwa kila mmoja; lakini uchungu huu unaounguza nyoyo unaambatana na hamasa ya kimapinduzi, hasira takatifu, hisia ya kulipiza kisasi na kudai damu ya shahidi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, safari hii mji mtukufu wa Qom, Mama wa Miji ya Ulimwengu wa Kiislamu, makazi ya Bibi Mtukufu wa Ahlul-Bayt (as), mji mkuu wa elimu, fiqhi, ijtihadi, ari ya kimapinduzi na uaminifu kwa Wilayah, utashuhudia utukufu mwingine wa kipekee.

Kila kitu kiko tayari kwa maandamano ya heshima ya kumuaga Bwana

Kila kitu kiko tayari kwa maandamano makubwa ya kumuaga Kiongozi Shahidi. Mji ambao ndio chimbuko la Mapinduzi Matukufu ya Kiislamu umevaa mavazi ya maombolezo ili kumsindikiza mwana wake shujaa, jasiri, mwenye hekima na aliyekulia katika Hawza ya Elimu ya Kiislamu, na kuupokea ukurasa mpya wa historia.

Hatimaye wakati uliokuwa ukisubiriwa wa ziara ya mwisho ya Bwana Shahidi katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran na kukutana Umma wa Kiislamu na kiongozi wao katika mji wa Bibi Mtukufu wa Ahlul-Bayt (Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake) umefika. Hakika nyakati hizi ni za uchungu mkubwa kwa wote; lakini uchungu huu wenye kuunguza nafsi unaambatana na hamasa ya kimapinduzi, hasira takatifu, hisia ya kulipiza kisasi na kudai damu ya shahidi.

Katika majonzi yako, viumbe wa ulimwengu watajipaka udongo vichwani mwao; na kwa macho yanayotiririka damu ya machozi, wataendeleza majonzi ya msiba huu.

Baada ya siku 127 za shauku na majonzi, wananchi wenye maombolezo kutoka pembe zote za Iran na hata kutoka nchi nyingine wamewasili Qom na katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran kwa ajili ya kumuona na kumuaga kwa mara ya mwisho Kiongozi wao Shahidi, ili wapunguze huzuni zilizomo nyoyoni mwao, wamlie kwa machozi na kufanya maombolezo.

Ewe Sahib az-Zaman (aj), tumempoteza baba yetu; sisi ni wenye nyoyo zilizovunjika, tuombee dua.

Usiku wa kihistoria katika kituo cha wanaomsubiri Mwokozi

Huku bado zikiwa zimesalia takribani saa saba kabla ya kuswaliwa mwili mtukufu wa Bwana Shahidi, Imam Khamenei, Msikiti Mtukufu wa Jamkaran na viwanja vyake tayari vilikuwa vimejaa wapenzi na wafuasi wa Wilayah. Karibu maeneo yote yamejaa watu, na kila dakika wimbi la waombolezaji liliendelea kuongezeka.

Dakika chache kuanzia (saa 11:00 usiku wa tarehe 15 Tir 1405), hafla ya kumuaga Imam Shahidi wa Umma ilianza kwa ushiriki usio wa kawaida wa wananchi wa kimapinduzi, waaminifu na walioitikia wito katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran. Wapenzi, waumini, wadai wa damu na wanaotaka kulipiza kisasi cha damu yake walisubiri kwa hamu ili waushike mwili mtukufu wa Bwana na Kiongozi wao mikononi mwao na kumuaga kihistoria Imamu wao.

Wapenzi na waliompenda Kiongozi Shahidi walikuja huku wakipaza kauli mbiu ya "Lazima Tusimame", na kwa ishara ya "ngumi zilizokunjwa", ili wakutane na kumuaga Bwana Shahidi wa Iran katika ziara yake ya mwisho kwenye Msikiti Mtukufu wa Jamkaran, mahali pa miadi ya wanaosubiri kudhihiri kwa Mwokozi.

Kupeperushwa kwa bendera ya kulipiza kisasi na kudai damu ya Bwana Shahidi

Bendera nyekundu zenye kauli "Yā Lithārāt al-Husayn" na "Yā Lithārāt al-Khamenei" zimepandishwa na wadai wa damu ya Bwana Shahidi katika Msikiti wa Jamkaran. Waombolezaji kwa sauti moja walipaza kauli "Kifo kwa Marekani" na "Kifo kwa Israel", huku wakisisitiza kulipiza kisasi cha damu ya Kiongozi wao na mashahidi wengine wapendwa.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Saa 3:30 alfajiri, Jumanne tarehe 16 Tir

Muda huo, aya za Qur'ani Tukufu zilisomwa mbele ya mkusanyiko wa wapenzi wa Kiongozi Shahidi wa Umma katika Msikiti wa Jamkaran, saa chache kabla ya kuswaliwa mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi.

Baada ya muda mfupi, Bwana wetu Shahidi alifika kwa mara ya mwisho katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran ili wafuasi wake waaminifu wamuage na kuusindikiza mwili wake mtukufu.

Mafuriko ya watu yamejaa katika viwanja vya Msikiti Mtukufu wa Jamkaran na barabara zinazouzunguka. Waombolezaji wanajipiga vifua na kulia kwa uchungu juu ya Kiongozi wao Shahidi; machozi ambayo yamechanganyika na hamasa ya Wairani pamoja na hasira takatifu ya kulipiza kisasi.

Kuanzishwa kwa mawakibu 2,000 ya huduma

Kwa mujibu wa viongozi wa maandalizi ya hafla ya kuaga na mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Umma, takribani mawakibu 2,000 zilindaliwa kwa ushirikiano wa wananchi na wanazuoni zimewekwa katika njia kuu ya matembezio ya mazishi, maeneo yanayozunguka Msikiti Mtukufu wa Jamkaran, Haram Tukufu ya Bibi Fatimah Ma'sumah (as) na katika barabara za mji mtukufu wa Qom ili kuwahudumia mazuwari wa Shahidi wa Ramadhani na wa Walii wa jambo la Waislamu.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Saa 4:10 alfajiri, Jumanne

Mda huo, mafuriko ya wapenzi na waliompenda Kiongozi Mujahid Shahidi yalianza kutoka Haram Tukufu ya Bibi Fatimah Ma'sumah (as) kupitia Barabara ya Mtume Mkuu (saww), ili kuusindikiza mwili wa shujaa mkubwa aliyetoa maisha yake yote katika kulinda Uislamu, Mapinduzi na heshima ya Iran ya Kiislamu.

Njia zote zinazoelekea kwenye Barabara ya Kiroho ya Mtume Mkuu (saww) na Msikiti Mtukufu wa Jamkaran zimefungwa, na wananchi waaminifu wanasonga mbele kwa taratibu ili wafike katika eneo kuu la kuaga na kukutana kwa mara ya mwisho na Imam wao Shahidi.

Saa 4:30 alfajiri – Kusomwa kwa Dua ya Ahad

Wakati huo sehemu za Dua ya Ahad zilisomwa katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran, saa chache kabla ya kuswaliwa mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi, kwa sauti ya msomaji wa mashairi ya Ahlul-Bayt wa Ismah na Twahara, Hajj Abbas Heydarzadeh. Wanaosubiri kudhihiri kwa Imam wa Zama wamezitoa thawabu ya dua hiyo kwa roho tukufu ya Bwana Shahidi na mashahidi wote wapendwa.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Saa 5:05 – Mlio wa kauli mbiu “Lazima Tusimame”

Utenzi maarufu wa maombolezo “Lazima Tusimame” uliimbwa na Hajj Mohsen Muhammadi-Panah saa chache kabla ya kuswaliwa mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi, na sauti yake ikavuma katika anga za Msikiti Mtukufu wa Jamkaran.

Wananchi waliokuwa katika maombolezo, wakiwa wamebeba bendera nyekundu zenye kauli “Yā Lithārāt al-Husayn” na “Yā Lithārāt al-Khamenei”, walidai kulipiza kisasi kikubwa dhidi ya Trump mhalifu na Netanyahu muuaji wa watoto.

Saa 5:30 asubuhi – Kuwasili kwa Ayatullah al-Udhma Jawadi Amuli

Muda huo, Ayatullah al-Udhma Jawadi Amuli, miongoni mwa Marajii wakubwa wa taqlidi, aliingia katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran na kufika kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili ya kuswaliwa swala ya maiti juu ya mwili safi na mtukufu wa Imam Shahidi pamoja na mashahidi wapendwa wa familia yake.

Saa 5:35 – Kuwasili kwa Ayatullah Shab Zindehdar

Ayatullah Muhammad Mahdi Shab Zindehdar, Katibu wa Baraza Kuu la Hawza za Elimu za Kiislamu nchini na mjumbe wa Mafuqaha wa Baraza la Walinzi, naye muda mfupi uliopita aliwasili katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran kwa ajili ya kushiriki katika hafla hii kubwa na ya kihistoria ya kumuaga na kumsindikiza shahidi mtukufu wa Umma wa Kiislamu. Akiwa pamoja na Wairani wenye huzuni na waliotengeneza historia hii, alijiunga na bahari kubwa ya umati wa waombolezaji na wanamapinduzi.

Saa 5:45 – Kuwasili kwa Ayatullah Arafi

Ayatullah Arafi, Mkuu wa Hawza za Elimu za Kiislamu nchini na mjumbe wa Mafuqaha wa Baraza la Walinzi, naye aliwasili katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran kwa ajili ya kumuaga, kumsindikiza na kufanya mkutano wa mwisho na Marjii Mujahid, Walii wa Jambo la Waislamu, Bwana Shahidi Ayatullah al-Udhma Khamenei (Quddisa Sirruhush-Sharif), na akatoa heshima zake kwa mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi.

Saa 5:50 asubuhi – Ayatullah Jawadi Amuli aubusu kilemba cha Bwana Shahidi

Ayatullah Jawadi Amuli, akiwa amefika karibu na mwili mtukufu wa Shahidi mpendwa, Ayatullah al-Udhma Imam Khamenei (Quddisa Sirruhush-Sharif), pamoja na mashahidi wa familia yake, alitoa heshima zake kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Saa 6:05 – Kuswaliwa swala juu ya mwili mtukufu wa Imam Shahidi na mashahidi wapendwa

Kwa muda huo, swala juu ya mwili mtukufu wa Imam Shahidi na mashahidi wapendwa ilianza kwa uongozi wa Ayatullah Jawadi Amuli, mbele ya mamilioni ya wapenzi wa Kiongozi Shahidi katika Msikiti Mtukufu wa Jamkaran. Machozi ya Ayatullah Jawadi Amuli yalitiririka wakati wa kuswali swala hiyo, huku macho yake yakiwa yamejaa huzuni na machozi.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Saa 6:20 – Kuanza kwa hafla ya kumsindikiza na mazishi ya Walii wa Amri Shahidi

Baada ya kuswaliwa swala na Ayatullah Jawadi Amuli, miili mitukufu ya Imam wa Waislamu, Ayatullah al-Udhma Khamenei (Quddisa Sirruhush-Sharif), pamoja na watu wengine wa familia yake waliouawa kishahidi, iliwekwa juu ya mikono ya wananchi wanamapinduzi na wale waliotengeneza utamaduni wa kujitoa mhanga kwa ajili ya mashahidi, na kuanza safari ya maandamano ya mazishi.

Hafla ya kumuaga na kumsindikiza Bwana Shahidi inafanyika kupitia Barabara ya Mtume Mkuu (saw) kuelekea Haram Tukufu ya Bibi Fatimah Ma'sumah (as).

Kutiririka kwa bahari ya umati wa waombolezaji, lakini wenye uimara na kuvunja nguvu za maadui

Bahari ya umati wa waombolezaji, lakini wenye msimamo, wenye fahari na watengeneza historia, imetapakaa katika njia ya kumuaga na kumsindikiza Bwana Shahidi kutoka Msikiti Mtukufu wa Jamkaran hadi Haram Tukufu ya Bibi Fatimah Ma'sumah (Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake), huku wakipaza kwa sauti moja kauli “Labbaik Sayyid Mujtaba”.

Ripoti ya Dakika kwa Dakika ya Hafla ya Kuaga na Mazishi ya Imam Shahidi Jijini Qom/ Msimamo wa Wanaodai Damu ya Bwana Shahidi + Picha

Wamepaza kwa sauti moja kauli “Kulipiza kisasi! Kulipiza kisasi!”, na kauli yao moja imekuwa: “Kulipiza kisasi, kulipiza kisasi! Tutamuua, tutamuua yule aliyemuua Imam wetu!”

Watu wasio Wairani kutoka mataifa mbalimbali nao wamekuja pamoja na familia zao katika hafla hii ya mamilioni ya watu, ili kufanya upya ahadi yao kwa Imam na Kiongozi wa Waislamu, na kumwambia: “Wako juu ya ahadi ile waliyoitoa.”

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha