Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Matembezi hayo yaliwahusisha mamia ya waumini waliokuwa wamevalia mavazi meusi ya maombolezo huku wakibeba mabango yenye ujumbe wa amani, uadilifu na kupinga dhuluma. Washiriki walisisitiza kuwa ujumbe wa Imam Hussein (as) unaendelea kuwa chanzo cha msukumo katika kusimamia haki, kupigania utu wa binadamu na kusimama dhidi ya dhuluma katika kila zama.
Aidha, viongozi wa dini walieleza kuwa maadhimisho ya Ashura si tukio la maombolezo pekee, bali ni fursa ya kujifunza maadili ya kujitolea, subira, uadilifu na kujenga jamii yenye mshikamano na amani.
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |











Maoni yako