Jumapili 31 Mei 2026 - 16:20
Naibu Waziri Mkuu wa Imarati aunga mkono mashambulizi dhidi ya Mashia nchini Bahrain

Hawza/ “Fahd Al-Amiri”, balozi wa Imarati nchini Bahrain, aliwasilisha barua iliyoandikwa kutoka kwa “Saif bin Zayed Al Nahyan”, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Imarati, kwa “Rashid Abdullah Al Khalifa”, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Bahrain.

Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjuma cha Shirika la Habari la Hawza, “Fahd Al-Amiri”, balozi wa Imarati nchini Bahrain, aliwasilisha barua iliyoandikwa kutoka kwa “Saif bin Zayed Al Nahyan”, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Imarati, kwa “Rashid Abdullah Al Khalifa”, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Bahrain.

Barua hiyo ilijumuisha pongezi kutoka kwa Waziri wa Imarati kutokana na juhudi za kiusalama za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Bahrain, na ilielezea mshikamano wa Imarati na Bahrain, pia ilisisitiza kuunga mkono hatua zote zinazochukuliwa na nchi hiyo kwa ajili ya kuhifadhi mamlaka yake ya kitaifa, usalama na uthabiti wake, na ikapongeza utendaji wa vyombo vya usalama vya Bahrain pamoja na taaluma yao katika kukabiliana na mipango yote.

Pande hizo mbili katika mkutano huo zilijadili nyanja za ushirikiano wa kiusalama, masuala yanayohusiana na kuendeleza shughuli za pamoja kati ya nchi hizo mbili hasa katika sekta ya usalama, pamoja na maendeleo ya karibuni ya hali ya kikanda.

Haya yanajiri wakati ambapo mashirika ya haki za binadamu yamesisitiza kuwa: Bahrain na Kuwait zimetumia “vita vya kikanda” kama kifuniko cha kampeni za ukandamizaji zilizopangwa.

Hatua hizi tangu kuanza kwa vita vya kikanda zimejumuisha kukamatwa kwa watu wengi miongoni mwa Waislamu wa madhehebu ya Shia, kunyang’anywa uraia kwa mamia ya wapinzani, wanazuoni wa dini, waandishi wa habari na wanaharakati, pamoja na matumizi ya mbinu ya “kupoteza watu kwa nguvu” na kuhalalisha kuwa kosa uhuru wa kujieleza kupitia mtandao.

Nchi hizi baada ya watu waliotajwa kukataa uchokozi wa Marekani na Wazayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutoa wito wa kumalizwa kwa uwepo wa kijeshi wa Marekani katika nchi za eneo hili, zimewatuhumu kwa mashtaka kama mshikamano na Iran na kuhusishwa na fikra ya “Wilayat al-Faqih.”

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha