Jumatano 20 Mei 2026 - 13:00
“Shahidi Raisi” alikuwa mfano wa utawala wa kidini na wa wananchi/ Rais shahidi hakuwa kabisa mtu wa kutafuta umaarufu wa kisiasa

Hawza/ Shahidi Raisi alikuwa mtu mwenye kujitolea na mwenye imani, ambaye katika aina yake ya utawala na siasa hakuwaza chochote isipokuwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu na kuitikia maelekezo na matakwa ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi, katika njia hii takatifu pia, kupitia shahada yake, alipata daraja bora zaidi la kibinadamu.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, kulea na kuitambulisha jamii nyuso mashuhuri na zenye kujitolea kama Ayatullah Shahidi Sayyid Ibrahim Raisi ni miongoni mwa matunda na baraka za Mapinduzi ya Kiislamu na harakati za fikra na utamaduni za Maimamu wawili wa Mapinduzi, jambo ambalo bila shaka vipengele vyake mbalimbali vinapaswa kuchunguzwa na kutathminiwa kwa usahihi na kitaalamu.

Imamu na Kiongozi wetu Shahidi, mwezi pili mwaka uliopita, katika mkutano na familia za mashahidi wa huduma, aligusia jambo muhimu kuhusu suala hili ambalo leo linamfanya mtu kutafakari zaidi kuliko wakati mwingine wowote, katika kikao hicho, pamoja na kupongeza huduma za kudumu za Shahidi Raisi, alitumia ibara ya “uwezo wa mapinduzi wa kutengeneza watu”, kisha akaeleza kwamba; Mapinduzi ya Kiislamu yana uwezo na vipawa vya kulea watu na kuitambulisha jamii watu walio katika kiwango cha mashahidi kama Raisi na Soleimani.

Rais Shahidi katika huduma ya malengo ya kimapinduzi ya taifa

Dkt. Mahdi Eslami, mjumbe wa jopo la kitaaluma katika Taasisi ya Utafiti ya Imam Sadiq (as), alisema: Shahidi Raisi kwa hakika alikuwa katika kiwango cha rais wa kimapinduzi na mwenye kushikamana na Wilayah; kwa muda wa karibu miaka mitatu alifanya kazi na juhudi “kwa ajili ya Iran”, hakuchoka, alisafiri kutoka jimbo moja hadi jingine, na alijitahidi sana ili kwa nafasi yake aweze kutatua sehemu ya matatizo na changamoto za wananchi.

Akiashiria kwamba katika njia ya kuhudumia maadili ya Mapinduzi ya Kiislamu na malengo ya taifa tukufu la Iran hakupuuza juhudi yoyote, aliongeza: Shahidi Raisi alikuwa mtu mwenye kujitolea na mwenye imani ambaye katika aina yake ya utawala na siasa hakuwaza chochote isipokuwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu na kuitikia kauli na matakwa ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi, licha ya kwamba miaka miwili imepita tangu shahada yake, bado hotuba ya rais shahidi katika kikao cha mwisho cha Baraza la Mawaziri iko hai katika kumbukumbu, ambapo kwa kutegemea matakwa ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi alisema kwamba; atajiepusha na kuibua masuala yatakayosababisha hitilafu baina ya mihimili ya dola, kwa hakika alikuwa mkweli kwa watu na kwa Kiongozi Shahidi katika matendo na maneno yake, na hatimaye kupitia shahada katika njia ya Mwenyezi Mungu na huduma kwa wananchi, alipokea malipo ya uongozi wake wa kijihadi.

Mfano wa utawala wa kidini na wa wananchi

Mhadhiri huyu wa chuo kikuu pia alisema kwamba, juhudi za dhati na zisizochoka za shahidi huyu mtukufu, iwe katika kipindi cha kazi katika mfumo wa mahakama, au katika huduma kama msimamizi wa Haram ya Quds Razavi, na hasa katika kipindi cha miaka mitatu ya urais wake, zimeacha alama na sifa zenye thamani katika uga wa “utawala wa kidini na wa wananchi”.

Alisema: Katika aina hii ya utawala, jambo lililo wazi ni kwamba; kiongozi na msimamizi licha ya ugumu wote, mashinikizo na vikwazo, hasubiri bajeti, bali kwa mtazamo wa kijihadi na usimamizi wa kiakili hujitahidi hata kubadilisha vitisho vilivyopo mbele yake kuwa fursa, bila shaka, uundaji huu wa fursa hupatikana kupitia mtazamo na fikra tukufu za kidini.

Aliendelea kusema: Utawala wa kidini na wa wananchi ni dhana ambayo katika namna ya kushughulikia siasa na uongozi wa jamii, husisitiza zaidi misingi na maadili ya dini pamoja na ushiriki wa wananchi.

Kuwahudumia watu kwa uaminifu kwa lengo la kupunguza mateso na maumivu ya taifa ni miongoni mwa vipengele vyake vikuu, na kwa hakika katika kipindi cha urais wa Ayatullah Raisi tulishuhudia kudhihirika kwa jambo hili.

Kukabiliana kwa uwazi na ukweli na walioneemesha Mapinduzi

Eslami pia aliongeza: Shahidi Ayatullah Raisi, hasa katika safari zake za majimbo kwa lengo la kuondoa au kupunguza kiwango cha matatizo yaliyopo katika majimbo na maeneo mbalimbali ya nchi, hususan maeneo maskini na yaliyonyimwa huduma, alionyesha kwa watu wote sura ya utawala wa Kiislamu ambao kwa hakika ulikuwa miongoni mwa matarajio na malengo makubwa ya Maimamu wawili wa Mapinduzi.

Rais shahidi hakuwa kabisa mtu wa harakati za kujionesha

Dkt. Muhammad Sadiq Khorsand, mhadhiri wa chuo kikuu na mchambuzi wa masuala ya kisiasa, pia akirejelea kwamba kuzingatia wananchi kwa serikali ya kumi na tatu na rais shahidi hakukuwa kabisa harakati za kujionesha, alisema: Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu katika mojawapo ya mikutano yake na wajumbe wa Baraza la Mawaziri alitaja moja ya mazuri ya serikali ya kumi na tatu kuwa ni mawasiliano ya moja kwa moja na ya karibu na wananchi kupitia safari za majimbo, hili linaonyesha kwamba katika mfumo wa fikra zake, suala la kuzingatia wananchi na kukutana bila ya vizuizi na matabaka ya watu lilikuwa na umuhimu mkubwa sana.

Mtazamo wa kimaadili katika utawala

Alisema: Jambo jingine muhimu ni unyenyekevu na maadili ya Shahidi wa Jamhuri katika kipindi cha usimamizi wa kisiasa na kiutendaji wa nchi, na kwamba mwenendo huu hasa katika kushughulika na matabaka ya maskini na waliodhulumiwa katika jamii, unatokana na mtazamo wa kimaadili wa viongozi wakubwa wa dini yetu.

Mjumbe wa jopo la kitaaluma katika Taasisi ya Utafiti ya Imam Sadiq (as) pia alisema: Miongoni mwa vipengele vingine vya utawala wa kidini na wa wananchi vilivyodhihirika wazi katika aina ya siasa za Shahidi Raisi ni suala la uwazi na kuwajibika kwa wananchi, na kwamba wananchi wanapaswa kufahamishwa yanayoendelea huku viongozi wakiwa na mtazamo wa kimaadili katika kuwashawishi wananchi na kuwajibu kwa uwazi na ukweli.

Kushikamana na sheria na kupambana na ubaguzi

Aliongeza: Bila shaka kwa ajili ya kufikia malengo ya juu katika mwenendo huu, inahitajika utawala wa sheria na uadilifu; na kwamba viongozi kuanzia kileleni mwa serikali hadi chini wanapaswa kuwa na mshikamano na utiifu kwa sheria, huku mstari wao mwekundu ukiwa ni utekelezaji wa sheria kwa uadilifu bila ubaguzi, kiasi kwamba katika aina hii ya utawala na siasa, haki za umma zihifadhiwe na kuheshimu utu wa mwanadamu kusiwe tu kaulimbiu bali pia kutekelezwe kwa vitendo.

Mhadhiri huyo wa chuo kikuu pia alisisitiza: Utawala wa kiutendaji kwa mtindo wa Shahidi Raisi, ambao unatokana na malezi ya kidini na ya kimapinduzi ya shahidi huyu mpendwa katika anga ya Jamhuri ya Kiislamu kwa mujibu wa uelewa wa Maimamu wawili wa Mapinduzi, huonekana zaidi tunapofahamu kwamba miaka ya tisini katika fasihi ya Imamu na Kiongozi wetu Shahidi ilitajwa kama alama ya uzembe na kutokuwepo maendeleo, na juhudi za miaka mitatu za Shahidi Raisi zilisababisha kwa kiwango kikubwa tabasamu la ridhaa kuonekana katika nyuso za Imamu wa jamii na wananchi ambao ni walioneemesha Mapinduzi.

Juhudi zisizochoka za kuinua ufanisi wa mfumo

Aliongeza: Miongoni mwa sifa muhimu zaidi za siasa na utawala wa kidini na wa kimapinduzi zilizodhihirika kwa Shahidi Raisi ni suala la ufanisi na matokeo ya shughuli, na kwamba lengo hapa ni kutoa huduma kwa wananchi kwa mtazamo wa kuinua ubora na tija katika usimamizi wa mambo pamoja na kutatua matatizo na changamoto, ambapo katika suala hili pia madai ya wananchi yana nafasi muhimu, juhudi hizi ndizo zilizosababisha tushuhudie kuongezeka kwa kiwango cha ufanisi wa mfumo.

Khorsand mwishoni alisema: Rekodi ya Shahidi Raisi katika kipindi cha urais wake, licha ya kwamba kwa sababu ya shahada yake ilikuwa kwa muda mfupi kwa kiasi fulani, lakini njia na mwenendo wake ulikuwa amana na urithi ambao unaweza kutumiwa kwa kiwango cha juu katika kuendesha nchi, na ni lazima vipengele mbalimbali vya mtindo wake wa utawala katika jamii yetu ya kimapinduzi na Kiislamu vifafanuliwe kwa usahihi.

Ripoti: Sayyid Muhammad Mahdi Mousavi

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha