Ijumaa 13 Machi 2026 - 23:20
Mkutano wa Mtandaoni wa “Kongamano la Saba la Kimataifa la Qudsi Tukufu” umefanyika

Hawza/ Jumuiya ya Kimataifa ya Qadimun kwa kushirikiana na taasisi kadhaa za kimataifa imeandaa mkutano wa mtandaoni wa “Kongamano la Saba la Kimataifa la Qudsi Tukufu” kwa ushiriki wa wanazuoni na wanaharakati wa muqawama wa Palestina.

Kwa mujibu wa kitengo cha kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, Jumuiya ya Kimataifa ya Qadimun kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wanazuoni wa Iraq, Muungano wa Wanazuoni wa Muqawama, Jukwaa la Harakati ya Kiislamu ya Lebanon, Baraza la Wanazuoni wa Palestina, Taasisi ya Palestina ya Pakistan, Muungano wa Kimataifa wa Samidun, Muungano wa Redio na Televisheni za Kiislamu, Idara Kuu ya Waislamu ya Muungano wa Urusi, Naibu wa Masuala ya Kimataifa wa Hawza, Kamati ya Utamaduni ya Arbaeen na Tume ya Haki za Binadamu ya Kiislamu ya London, ilifanya mkutano wa mtandaoni wa Kongamano la Saba la Kimataifa la Qudsi Tukufu siku ya Alhamisi.

Wazungumzaji walioalikwa katika hafla hii:

Ayatullah A’rafi; Mkurugenzi wa Hawza za Elimu za Kidini nchini Iran.
Sheikh Khalid al-Mulla; Rais wa Jumuiya ya Wanazuoni wa Uislamu wa Iraq.
Sheikh Maher Hammoud; Rais wa Muungano wa Wanazuoni wa Muqawama kutoka Lebanon.
Sheikh Zuhair Ja’id; Rais wa Jukwaa la Harakati ya Kiislamu ya Lebanon
Sheikh Hussein Qasim; Rais wa Baraza la Wanazuoni wa Palestina.
Sheikh Kifah Batta; Mufti wa Urusi
Dkt. Azmi Abdul Hamid; Rais wa Mashirika ya Kiislamu ya Malaysia
Sharafuddin Kilic; Mwakilishi wa Bunge la Uturuki
Dkt. Mustafa Sand; Mwakilishi wa Bunge la Iraq.
Dkt. Noor Adel; Mwakilishi wa Bunge la Iraq.
Profesa Iqbal Kurpinar; Mhadhiri wa Chuo Kikuu na mwanaharakati wa meli ya “Sumud” kutoka Uturuki.
Dkt. Charlotte Kates; Mwanachama wa Taasisi ya Samidun na mmoja wa maprofesa waliofukuzwa kutoka Chuo Kikuu cha Marekani kutoka Kanada.
Dkt. Masoud Shajareh; Rais wa Tume ya Haki za Binadamu ya Kiislamu ya London.
Maryam Abu Daqqa; Mwanamuqawama wa Palestina aliyekombolewa na mwanachama wa bodi ya uhariri ya Harakati ya Wananchi wa Palestina.
Tushar Gandhi; Mwanaharakati wa Palestina.
Dkt. Khalid Saadi; Mwanachama wa Jukwaa la “A’idun” na Jukwaa la Ukombozi wa Wananchi wa Palestina kutoka Sweden.
Dkt. Abdulhafidh al-Sariti; Katibu wa Baraza la Harakati ya Kitaifa kwa Ajili ya Palestina kutoka Morocco.
Dkt. Rida Shiklar Oglu; Mhadhiri wa Chuo Kikuu na mwanaharakati wa meli ya “Sumud” kutoka Uturuki
Dkt. Brano Richa; Mwanaharakati wa Palestina na mwandishi wa habari kutoka Brazil.
Profesa Moiser Garcia; Mhadhiri wa Chuo Kikuu na mwanaharakati wa Palestina kutoka Mexico
Zainab al-Saffar; Mwandishi wa habari wa Al-Mayadeen kutoka Lebanon
Dkt. Saber Abu Maryam; Rais wa Taasisi ya Palestina kutoka Pakistan
Dkt. Ahmad Wehman; Rais wa Kituo cha Uangalizi cha Morocco cha Kupambana na Uhalalishaji wa Mahusiano (na Israel) kutoka Morocco

Mkutano huu ulioendeshwa na Hujjatul-Islam wal-Muslimin Rasul Baqeri, Katibu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Qadimun, ulirusha matangazo yake moja kwa moja kupitia mitandao ya Muungano wa Redio na Televisheni za Kiislamu.

Mkutano wa Mtandaoni wa “Kongamano la Saba la Kimataifa la Qudsi Tukufu” umefanyika

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha