Jumatano 11 Februari 2026 - 23:00
Ayatullah A‘rafi ashiriki katika matembezi ya kuzivunja nguvu za adui ya 22 Bahman

Hawza/ Mkurugenzi wa Hawza nchini Iran, ameshiriki sambamba na wananchi wa kimapinduzi na wachamungu katika matembezi ya kishujaa na ya kuzivunja nguvu za adui ya tarehe 22 Bahman mjini Qum.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Alireza A‘rafi, Mkurugenzi wa Hawza, alishiriki pamoja na wananchi waaminifu, watiifu kwenye uongozi wa Wilaya, wenye utambuzi, wa kimapinduzi na wachamungu katika maandamano ya kishujaa na ya kuzivunja nguvu za adui ya 22 Bahman huko Qum.

Qum kwa mujibu wa maelezo ya Ayatullah A‘rafi, Mkurugenzi wa Hawza, ni “mji wa kidunia” (jahan-shahri) ambao ndani yake wapo watu wa makabila, rangi na mataifa mbalimbali. Katika siku ya muujiza wa Mwenyezi Mungu ya 22 Bahman pia, wazee na vijana, wanawake na watoto, Wakurdi na Waluri, Waarabu na Wabaluchi, Waturuki na Waajemi, Wairani na wasiokuwa Wairani, wote kwa pamoja wakiwa na kaulimbiu za “Mauti kwa Marekani”, “Mauti kwa Israel”, “Mauti kwa mchochezi wa fitina”, “Mauti kwa mnafiki”, “Damu iliyo katika mishipa yetu ni zawadi kwa kiongozi wetu”, “Sote ni askari wako ewe Khamenei, tupo chini ya amri yako ewe Khamenei”, “Haitatupata fedheha (Hayhat minna al-dhillah)” na kadhalika, walijitokeza katika medani ya kuitetea damu ya fidia ya mashahidi ili katika sherehe yenye upana wa Iran pendwa waoneshe umoja, mshikamano na maelewano ya kitaifa, na kuwafahamisha maadui hususan Marekani mhalifu na utawala wa Kizayuni muuaji wa watoto kwamba: “Hawawezi kufanya lolote.”

Katika siku ya kutangaza uaminifu na uungaji mkono wa umma kwa Mapinduzi ya kimataifa ya mtukufu Ruhullah, wote wamejitokeza uwanjani ili kuwaambia wenye nia mbaya na maadui wa Iran na Wairani kwamba; kwa kuitikia wito wa Bwana na Kiongozi wao, Hadhrat Imam Khamenei (Mwenyezi Mungu amhifadhi), wapo tayari kulinda urithi wa Mbunifu Mkuu wa Mapinduzi na damu ya mashahidi hadi tone la mwisho la uhai wao, na hawataruhusu dosari yoyote iingie katika utambulisho wao wa kimapinduzi. Na licha ya matatizo ya kiuchumi, wanasonga mbele kwa uthabiti zaidi kuliko zamani kuelekea kilele ambacho Walii wa Mambo ya Waislamu amekiahidi na kukibashiria, na kamwe hawatasimama.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha