Ijumaa 19 Desemba 2025 - 23:53
Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Hawza/ Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, ametunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini (ra), kutokana na kutambua mchango wake mkubwa katika kuhudumia Ummah wa Kiislamu, kutetea haki za watu waliodhulumiwa na wanyonge, pamoja na kusimamia na kueneza itikadi ya Imam Khomeini (ra).

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Tuzo hiyo ilikabidhiwa, tarehe 17 Desemba 2025, katika hafla rasmi iliyofanyika nchini Iran, huku wakishiriki wa viongozi mbali mbali wa kidini, kisiasa, kijamii na wawakilishi wa taasisi mbalimbali.

Kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hiyo, Sheikh Zakzaky anatambuliwa kama mmoja wa viongozi mashuhuri walioweka maisha yao wakfu katika kupigania haki, uadilifu wa kijamii na mshikamano wa Ummah, kwa kuzingatia misingi ya Mapinduzi ya Kiislamu yaliyoasisiwa na Imam Khomeini (ra). Tuzo hii ni ishara ya heshima na kuthaminiwa kimataifa, kutokana na mchango wake wa muda mrefu katika kuhamasisha uamsho wa Kiislamu na kusimama imara upande wa waliodhulumiwa.

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria, Sheikh Ibraheem Zakzaky, Atunukiwa Tuzo ya Dunia ya Imam Khomeini + Picha

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha