Alhamisi 11 Septemba 2025 - 15:26
Mashabiki wa Timu ya Italia Wapinga Wimbo wa Israel

Hawza/ Mashabiki wa timu ya mpira wa miguu ya Italia, wakati unaimbwa wimbo wa utawala wa Kizayuni, katika hatua ya ishara ya kupinga jinai za kikatili zinazofanywa na utawala huo, waliupa mgongo uwanja huo na kuinua mabango yaliyoandikwa “Simamisheni”.

Kwa mujibu wa ripoti ya Idara ya tarjuma ya Shirika la Habari la Hawza, mashabiki wa timu ya taifa ya Italia mara nyingine tena waligeuza nyuso zao na kugeukia nyuma wakati wimbo wa utawala wa Kizayuni unapigwa, timu ya Italia inashiriki katika michezo ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 katika kundi hili.

Tukio kama hili lilitokea pia mwaka 2024 wakati timu hizi mbili zilipokutana.

Aidha, barua rasmi kutoka Chama cha Makocha wa Michezo cha Italia imetumwa ikiitaka UEFA na FIFA kuiondoa na kuisimamisha timu ya Israel katika mashindano ya kimataifa ya michezo kutokana na jinai za kibinadamu ambazo utawala huo bandia umekuwa ukizifanya huko Ghaza na Palestina.

Chanzo: Football Italia

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha