Jumapili 6 Julai 2025 - 15:53
Hafla ya maombolezo ya usiku wa Ashura ya Husseini (as) katika Husainia ya Imam Khomeini huku ikihudhuriwa na Kiongozi wa Mapinduzi

Hawza/ Wakati huo huo na usiku wa Ashura ya Husseini (as), hafla ya maombolezo ilifanyika katika Huseinia ya Imam Khomeini (ra) huku ikihudhuriwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Mtukufu Ayatollah Khamenei pamoja na kundi la watu wa tabaka mbalimbali.

Kwa mujibu wa ripoti ya  Shirika la Habari la Hawza,, katika hafla hii Hujjatul-Islam  Mas'ud 'Ālī alitoa hotuba ambayo ilielezea funzo la harakati ya Imam Hussein (as) kuhusiana na kusimama kidete pamoja na kustahimili dhulma. Alilitaja taifa la Kiislamu la Iran kuwa ni mhimili wa upande wa kimataifa wa muqawama chini ya uongozi wa Waliyyu Amr al-Muslimin (Kiongozi wa Waislamu), na akasisitiza kuwa Uzayonisti wa kimataifa ndio mhimili mkuu wa upande wa batili.
Alisema pia: “Taifa la Iran, kwa mujibu wa mafunzo ya Ashura, halitowahi kujisalimisha kwa upande wa batili; kwa sababu kauli mbiu ya "Uwe mbali kwetu ni udhalili" 'هیهات منا الذلة' ndilo somo lifuatwalo.”

Katika mwendelezo wa hafla hii, Bwana Mahmoud Karimi alisoma mashairi na maombolezo kwa ajili ya kumuomboleza Bwana wa Mashahidi, Abā 'Abdillāh (as), na mashujaa wenzake waliouawa kishahidi, akifanya marthiya (tenzi za maombolezo) kwa hisia na huzuni.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha