Kwa mujibu wa ripoti ya Kitengo cha Tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, takriban miezi miwili baada ya utawala wa Kizayuni kukiuka makubaliano ya usitishaji vita, utawala huu wa kiuaji ulianzisha vizuizi vya kipekee na vya kinyama dhidi ya Ghaza, na ulifunga kabisa njia zote za mipakani kwa misaada ya kibinadamu, kama vile: maji, chakula, mafuta na dawa.
Kwa mujibu wa Mpango wa Chakula Duniani (WFP), hifadhi zote za chakula huko Ghaza zilimalizika mwezi Aprili 2024, na hali hiyo tangu mwezi Machi ilikuwa tayari imegeuka kuwa janga. Hata majiko yaliyo fadhiliwa kutoa misaada, ambayo kwa wastani yalikuwa yakipika zaidi ya milo milioni moja kwa siku, hayana chakula tena. Na vyakula vilivyobakia vimepanda bei kwa asilimia "1400", hali ambayo imenifanya ununuzi wake kuwa jambo lisilowezekana kabisa.
Maoni yako