Alhamisi 27 Februari 2025 - 10:37
Ushauri wa Imamu Ridha (AS) kuhusu siku za mwisho za Mwezi wa Sha'ban

Hadhrat Ayatollah Al-Udhma Sayyid Musa Shubairi Zanjani amesema: Imam Reza (AS) aliamuru kusoma sana dua hii katika siku za mwisho za Mwezi wa Sha'ban: «Ewe Mwenyezi Mungu! Ikiwa haujatusamehe hadi sasa katika sehemu iliyopita katika Mwezi huu, basi tusamehe katika sehemu iliyobakia ya Mwezi huu.»

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Hadhrat Ayatollah Al-Udhma Sayyid Musa Shubairi Zanjani katika hotuba yake alitaja riwaya ya ushauri wa Hadhrat Imam Ridha (amani iwe juu yake) kuhusu siku za mwisho za Mwezi wa Sha'ban, ambapo alisema:

Soma sana dua hii katika muda uliosalia wa Mwezi wa Sha'ban:

«اَللّهُمَّ اِنْ لَمْ تَکُنْ غَفَرْتَ لَنا فیما مَضی مِنْ شَعْبانَ فَاغْفِرْ لَنا فیما بَقِیَ مِنْهُ»

Ewe Mwenyezi Mungu! Ikiwa haujatusamehe hadi sasa katika sehemu iliyopita katika Mwezi huu, basi tusamehe katika sehemu iliyobakia ya Mwezi huu!.
Ni kweli kwamba Mwenyezi Mungu huwakomboa waja wengi kwa kuwakweka mbali na Moto wa Jahanamu katika Mwezi huu (wa Sha'ban).

Wasail al-Shia, Juzuu ya 10, uk wa 302.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha