Kwa mujibu wa Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, kikinukuu Shirika la Habari la Anadolu, vyanzo vya Kipalestina vimetangaza kuwa jeshi la utawala wa Kizayuni, wakati wa uvamizi wake katika mji wa Tal ulioko magharibi mwa Nablus, limewakamata zaidi ya vijana 40 wa Kipalestina.
Kwa mujibu wa ripoti ya Redio ya Palestina, wanajeshi wa Kizayuni bado wanaendelea na operesheni zao katika mji huo, huku wakifanya upekuzi katika makumi ya nyumba za raia.
Ripoti hiyo pia imeeleza kuwa vikosi vya uvamizi vimeteka moja ya nyumba za raia na kuigeuza kuwa kituo cha muda cha kuwahoji watu waliokamatwa.
Jeshi la utawala wa Kizayuni limeuzingira mji huo kutoka pande zote, na hadi sasa limeendelea kuweka vikwazo vikali vya usafiri na harakati katika eneo hilo.
Maoni yako