Jumapili 19 Julai 2026 - 14:00
Malaysia Yatangaza Kuwafukuza Raia wa Israel

Hawza/ Waziri Mkuu wa Malaysia ametangaza kwamba endapo raia wa Israel watabainika kuwepo nchini humo, watafukuzwa mara moja, kwa kuwa Malaysia haiutambui rasmi utawala wa Israel.

Kwa mujibu wa Kitengo cha Habari za Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, kikinukuu Islami Analysis, Anwar Ibrahim, Waziri Mkuu wa Malaysia, ametangaza kuwa; ikiwa raia wa Israel watagunduliwa ndani ya nchi hiyo, watafukuzwa mara moja, kwa sababu Malaysia haiutambui utawala wa Israel.

Kwa mujibu wa gazeti la ndani la Malay Mail, Anwar Ibrahim alitoa kauli hiyo akijibu taarifa zilizodai kwamba baadhi ya raia wa Israel wamegunduliwa nchini Malaysia, alisema kuwa taasisi zote za usalama za nchi hiyo zimeanza uchunguzi wa kina kuhusu madai hayo.

Alisema: "Tunachunguza suala hili na hatutaruhusu hali kama hiyo iendelee, ikiwa raia wa Israel watakuwepo nchini, kwa kuwa hatuitambui Israel, watafukuzwa mara moja."

Kauli ya Waziri Mkuu wa Malaysia imetolewa baada ya kuchapishwa kwa taarifa zilizodai kuwa baadhi ya raia wa Israel waligunduliwa katika jimbo la Johor wakitumia nyaraka za utambulisho zinazothibitisha uraia wa nchi mbili.

Malaysia na Israel hazina uhusiano wowote rasmi wa kidiplomasia, kwa mujibu wa sheria za Malaysia, wenye pasi za kusafiria za Israel hawaruhusiwi kuingia nchini humo isipokuwa wapate kibali cha maandishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Malaysia.

Vilevile, raia wa Malaysia hawaruhusiwi kusafiri kwenda Israel, na katika pasi za kusafiria za Malaysia kuna maneno yanayosema: "Pasi hii ya kusafiria ni halali katika nchi zote duniani isipokuwa Israel."

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha