Alhamisi 9 Julai 2026 - 15:04
Video | Sheikh Ibrahim Zakzaky Awasili Mashhad Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran

Hawza/ Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria, Sheikh Ibrahim Zakzaky, amewasili muda mfupi uliopita katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mashhad, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwa ajili ya kushiriki katika shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran aliyedhulumiwa.

Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Kuwasili kwa Sheikh Zakzaky kunadhihirisha mshikamano wa viongozi na watu huru kutoka sehemu mbalimbali za dunia katika kushiriki maombolezo ya kumpumzisha kiongozi huyo, ambaye ameacha athari kubwa katika ulimwengu wa Kiislamu na harakati za kupigania uadilifu.

Tazama video ifuatayo inayoonesha wakati Sheikh Ibrahim Zakzaky akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mashhad kwa ajili ya kushiriki katika mazishi hayo ya kihistoria:

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha