Jumapili 4 Januari 2026 - 07:22
Ayatullah al-‘Udhma Nouri Hamadani apongeza utendaji kazi wa Ayatullah A‘raafi

Mtukufu Ayatullah Nouri Hamedani, akirejelea utendaji kazi wenye thamani kubwa wa Ayatullah A‘raafi kwenye uongozi wa Hawza, ametoa pongezi kwa kuandaliwa kwa kongamano kubwa la kumuadhimisha Ayatullah Mirzaay Naa’iniy — radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah A‘raafi, Mkurugenzi wa Hawza, alikutana na kufanya mazungumzo na Mtukufu Ayatullah Nouri Hamedani, na akawasilisha ripoti ya mipango na shughuli kuu za Hawza.

Katika mkutano huo, Mtukufu Ayatullah Nouri Hamedani, akielezea huduma zenye thamani kubwa za Ayatullah A‘raafi katika uongozi wa Hawza, alitoa pongezi zake kutokana na kuandaliwa kongamano la kumuadhimisha Ayatullah Mirzaay Naa’iniy — radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Mtukufu huyo pia alitaja hotuba ya Ayatullah A‘raafi aliyotoa huko Najafu Ashraf kuwa ni hatua inayostahiki katika kuitambulisha nafasi ya kielimu na kifiqhi ya Ayatullah Mirzaay Naa’iniy — radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha