Jumatatu 8 Desemba 2025 - 13:45
Hispania Inaunga Mkono Kuundwa kwa Kola ya Palestina

Hawza/ José Manuel Álvarez, Waziri wa Mambo ya Nje wa Hispania, amekiri kwamba: ghasia za walowezi wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi zimevuka mipaka ya udhibiti. Sisi tunatambua rasmi kuundwa kwa dola ya Palestina.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Bw. Álvarez aliongeza kuwa: tumekosolewa sana kwa sababu ya kuitambua rasmi nchi ya Palestina, lakini hatua hii tumeichukua kwa misingi ya haki na utu wa kibinadamu mbele ya watu wa Palestina, na dunia inapaswa kulijua hilo.

Amesisitiza akisema: wakati wa kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina umewasili, na hili linahitaji Ukingo wa Magharibi na Ghaza kuwa chini ya serikali moja, viwe vimeungana na kuwa chini ya usimamizi wa dola huru moja.

Chanzo: WAFA

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha