Jumamosi 9 Agosti 2025 - 19:08
Athene Yaonyesha Wasiwasi Kuhusu Utaifishwaji Usio Halali wa Makanisa ya Ukingo wa Magharibi na Utawala Bandia wa Israel

Hawza/ Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya eneo la Ukingo wa Magharibi, makanisa ya Orthodox ya Kiyunani na mali zinazohusiana nayo katika eneo hilo yametaifishwa kinyume cha sheria na utawala wa jinai wa Kizayuni.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha  Shirika la Habari la Hawza, taarifa zinaonyesha kuwa wahamiaji haramu wa Kizayuni wanajihusisha na utaifishaji wa kutisha wa mali za makanisa ya Orthodox, hasa katika eneo la Ukingo wa Magharibi.

Miongoni mwa makanisa yaliyotaifishwa, ni Kanisa la kihistoria la Mtakatifu Gerasimos lililoko karibu na mji wa Yeriko, kwa mujibu wa ushahidi, mvutano katika eneo la Yeriko umeongezeka sana katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, na kuna uwezekano wa mali nyingine pia kutwaliwa kinyume cha sheria na wahamiaji haramu wa Kizayuni.

Katika muktadha huo huo, kikao cha dharura cha uchambuzi na ufuatiliaji kimefanyika mjini Athene ili kuchunguza na kutathmini hali ya ugawaji haramu wa ardhi za makanisa huko Baitul Muqaddas.

Chanzo: Shirika la Habari la Anadolu

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha