Jumanne 8 Julai 2025 - 11:21
Matembezi ya Ashura mwaka huu Arusha yavunja rekodi

Hawza/ Jiji la Arusha yamefanyika matembezi yaliyo fana mwaka huu, matembezi ambayo hayajawahi tokea katika miaka iliyopita.

Kwa mujibu wa  Shirika la Habari la Hawza Matembezi yaliyofanyika mwaka huu Jijini Arusha Tanzania yamefana kuliko miaka yote iliyopita, ukizingatia kwamba jiji la Arusha ni miongoni mwa miji ambayo imetekwa na fikra za kihabi nchini tanzania, lakini Ashura ya Imam Husein mwaka huu imelidhihirisha hilo katika sura ya tofauti baada ya kushuhudia umati mkubwa ambao ulitiririka barabarani kwa ajili ya kumuenzi na kumkumbuka Imam huyo.

Matembezi ya Ashura mwaka huu Arusha yavunja rekodi

Baadhi ya masheikh mbali mbali ambao walishiriki katika matembezi hayo

Umati huu unadhihirisha wazi kwamba madhehebu ya Ahlulbayt (as) katika jiji hilo yanaenea kwa kasi tofauti kabisa na miaka ya hivi karibuni, matembezi hayo yaliyofanyika yaliandaliwa na Huseinia ya Imam Ridha (as), Tasisi ya Katamul-Anbiya pamoja na Taasisi ya Ahlylbayt Center.

Matembezi ya Ashura mwaka huu Arusha yavunja rekodi

Sehemu ya waumini wa kike ambao walishiki kikamilifu katika matembezi hayo

Matembezi ya Ashura mwaka huu Arusha yavunja rekodi

Sehemu nyengine ya waumini wakike ambao waliweza kushiriki katika maombolezo hayo

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha