Jumapili 22 Juni 2025 - 23:47
Himaya Thabiti kutoka katika Kundi la Maulamaa, Wataalamu, na Walimu wa hawza ya Qum, kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu

Hawza/ Maulamaa, wataalamu na walimu arobaini wa hawza ya Qum, wakilaani mashambulizi ya kikatili yaliyofanywa na utawala dhalimu wa Kizayuni na kuonyesha uungaji mkono wa dhati kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, wamesisitiza kuwa: tunatoa onyo kali kuhusu athari mbaya na hatari sana zitakazotokana na vitisho vya kihaini na visivyo na haya dhidi ya Kiongozi Mkuu, na tunatoa wito kwa Waislamu wote duniani kulaani vitendo hivyo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, taarifa ya pamoja ya maulamaa, wataalamu na walimu wa hawza kuhusu kulaani mashambulizi yaliyofanywa na utawala dhalimu wa Kizayuni na kumuunga mkono kwa nguvu Kiongozi Mkuu, imeeleza kama ifuatavyo:

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu

Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu wote, rehma na amani zimshukie Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na Ahlul-Bayt wake watukufu.

Kauli Yake (Mwenyezi Mungu):

(َوَکَانَ حَقًّا عَلَیْنَا نَصْرُ الْمُؤْمِنِینَ)

“Na ilikuwa ni haki juu Yetu kuwanusuru Waumini.”

Katika muktadha wa mashambulizi ya kikatili na ya kijinga yanayoendelea kufanywa na utawala dhalimu na muuaji wa Quds, kwa kushirikiana na kuungwa mkono kwa wazi au kwa siri na baadhi ya madola ya Magharibi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran—ambapo taifa la Iran limejibu kwa subira isiyo na mfano na kwa ujasiri mkubwa wa majeshi yake madhubuti na waja wake mashujaa—ambapo hayo yote yameongeza heshima na fahari ya taifa hili lenye subira, sasa mdhamini mkuu wa utawala huu dhalimu, kwa upumbavu na kiburi kisicho kifani, amewatolea wito watu wa Iran wajisalimishe na ameenda mbali zaidi kwa kumtishia kumuua Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei (hifadhi ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake).

Tunapenda kusema wazi:

Kwa nguvu zote na kwa msimamo thabiti, tunalaani kwa ukali kila aina ya vitisho vya aina hiyo, na tunatoa onyo kali kuhusu athari mbaya na hatari kubwa zitakazotokana na kauli hizo zisizo na haya. Tunatoa wito kwa Waislamu wote duniani kulaani matamshi hayo na kuchukua msimamo wa pamoja kuyakataa.

Bila shaka yoyote, taifa hili la Iran lenye subira na kusimama imara, likimtegemea Mwenyezi Mungu Mlipiza kisasi, na kwa kujishikamanisha na kivuli salama cha Imam Mahdi (a.f), litapata ushindi dhidi ya maadui wake.

Hakika mshikamano, umoja na kujitolea kwa wananchi waaminifu na waadilifu wa Iran, ambavyo vimeongezeka zaidi kufuatia mashambulizi haya ya kinyama, ni jambo la kupongezwa na linastahili kila aina ya heshima na pongezi. Pia, tunapenda kutoa shukrani na pongezi kwa vyama vyote, makundi mbalimbali na raia wa Iran kutoka kote duniani waliolaani mashambulizi haya ya kinyama na kuonyesha mshikamano wa dhati na ndugu zao Wairani; vivyo hivyo kwa maulamaa wa Kiislamu na serikali zilizolaani mashambulizi hayo—tunawashukuru sana.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha