Kwa mujibu wa ripoti ya Idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, katika Eid al-Adha, waislamu wa Marekani wameandaa mikakati ya kuifanikisha sherehe ambayo inajumuisha kutoa zawadi kwa watoto pamoja na mpango wa kusambaza nyama na chakula kwa watu wenye uhitaji.
Miongoni mwa shughuli za sherehe hii ni pamoja na kuswali Swala ya Jamaa siku ya Ijumaa tarehe 6 Juni. Vilevile, maeneo mengi pia yameandaa sherehe maalumu zenye dhamira ya kifamilia katika siku hiyo ya Idd.
Katika kila Eid al-Adha, familia za Waislamu wa Marekani hushiriki katika Swala ya Jamaa yenye hadhi kubwa na vilevile katika hafla zinazofanyika. Misikiti mingi huwa ni kitovu cha shughuli hizi na hushughulika na kupanga mipango ya sherehe hii.
Maoni yako