Alhamisi 3 Septemba 2026 - 10:27
Hadithi ya Leo | Kuwatimizia Watoto Ahadi Mnazo Waahidi

Hawzah/ Imam Musa al-Kadhim (as), katika riwaya moja, anasisitiza umuhimu wa kutimiza ahadi pamoja na kuzingatia kwa namna ya kipekee haki za watoto.

Shirika la Habari la Hawza, limechapisha riwaya ifuatayo kutoka katika kitabu Mizan al-Hikmah:

Imam Musa al-Kadhim (as) amesema:

«إِذَا وَعَدْتُمُ الصِّغَارَ فَأَوْفُوا لَهُمْ؛ فَإِنَّهُمْ یَرَوْنَ أَنَّکُمُ الَّذِینَ تَرْزُقُونَهُمْ، وَإِنَّ اللَّهَ لَا یَغْضَبُ بِشَیْءٍ کَغَضَبِهِ لِلنِّسَاءِ وَالصِّبْیَانِ.»

“Mnapowaahidi watoto jambo fulani, basi timizeni ahadi hiyo kwao; kwa sababu wao wanaona kwamba nyinyi ndio mnaowaruzuku. Na Mwenyezi Mungu hakasiriki kwa jambo lolote kama anavyokasirika kwa sababu ya wanawake na watoto.”

Chanzo: Mizan al-Hikmah, Juzuu ya 13, ukurasa wa 252.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha